Friday, July 24, 2015

UANDIKISHAJI BVR DAR WATAWALIWA NA CHANGAMOTO

1.Mwandikishaji wa daftari la majina ya wapiga kura(katikati) akisoma jina la mwananchi aliyehitajika kwenda kujiandikisha.
Mwandikishaji wa Daftari la Wapiga Kura (katikati) akisoma jina la mwananchi aliyehitajika kwenda kujiandikisha.
2.Wananchi wakisubiri kujiandikisha eneo la kituo cha Kijitonyama Mpakani 'B'maeneo ya Mori.
Wananchi wakisubiri kujiandikisha eneo la kituo cha Kijitonyama-Mpakani B. 3.Hapa wananchi wakitafakari hatma yao ya kujiandikisha.
Hapa wananchi wakitafakari hatma yao ya kujiandikisha. 4.Mwananchi aliyeenda kujiandikisha(kulia) akipigwa picha na kamera maalum kwa ajili ya kupata kitambulisho eneo la kituo cha Sinza Mori Dar.
Mwananchi aliyekwenda kujiandikisha (kulia) akipigwa picha na kamera maalum kwa ajili ya kupata kitambulisho eneo la Sinza- Mori, Dar. 5.Waamdikishaji wa BVR wakiwa katika mashine zao.
Waandikishaji wa BVR wakiwa katika mashine za za kuandikishia. 6.Hapa wananchi waliojitokeza siku ya leo wakiwa nje ya geti, huku ndani wakihudumiwa wananchi walioandikishwa majina yao jana katika kituo cha Shule ya Msingi Sinza-Maalum.
Wananchi waliojitokeza nje ya geti la Shule ya Msingi Sinza-Maalum kwa ajili ya kuanza kujiandikisha huku ndani wananchi walioandikishwa majina yao jana wakipatiwa huduma ya kuandikishwa. 7.Mwananchi aliyeenda kujiandikisha (kulia) akiweka vidole kwenye mashine ya kuchukua alama za vidole eneo la Kituo cha kujiandikisha cha eneo la Mlimani City Dar.
Mwananchi aliyekwenda kujiandikisha (kulia) akiweka vidole kwenye mashine ya kuchukua alama za vidole eneo la Mlimani City, Dar. 8.Hapa mwanamama akisaidiwa na mwandikishaji jinsi ya kukaa ili aweze kuchukulia picha eneo la kituo cha Sinza 'A'.
Mama mmoja, mkazi wa Sinza A akisaidiwa na mwandikishaji jinsi ya kukaa ili aweze kupigwa picha kwa ajili ya kitambulisho cha kupigia kura. 9....akichukuliwa picha.
....akipigwa picha. 10.Wananchi wakiwa katika foleni kusubiria kujiandikisha eneo la kituo cha Mlimani City Dar.
Wananchi wakiwa katika foleni kusubiria kujiandikisha maeneo ya Mlimani City, Dar.
IKIWA sasa ni siku ya tatu tangu zoezi la uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura uanze kwa  teknolojia ya Biometric Voters Regitration (BVR), hali imezidi tete baada ya wakazi wa Dar kupata usumbufu wa kuamka asubuhi na mapema kwenda kujiandikisha na kurudi bila mafanikio.
Mapema hii leo mwandishi wetu amefanikiwa kutembelea baadhi ya vituo kama vya Sinza, Shule ya Msingi Mapambano, Mwenge, Kijitonyama pamoja na maeneo ya Mlimani City Dar na kushuhudia umati mkubwa ukiwa kwenye foleni kwa ajili ya kujiandikisha.
Katika baadhi ya vituo hivyo, zoezi lilionekana likiendelea vizuri huku baadhi ya maeneo yakiwa na changamoto za wananchi kulalamikia ubovu ‘Solar power’ zinazotumika katika mitambo ya uandikishaji kuwa jua linapopungua na mitambo husimama kutokufanya kazi.
Kituo Cha Kijitonyama-Mpakani B, maeneo ya Mori wananchi wengi wamelalamikia foleni kuwa ndefu na zoezi kwenda taratibu, huku wakilalamikia suala la kuandikishwa majina kisha kupatiwa vitambulisho siku inayofuata.
“Tunaomba waandikishaji wa BVR wasilaze majina kwa kuwa inasababisha msongamano na vurugu kwa wananchi wanaojitokeza siku inayofuata tena wakiwa wameamka alfajiri kushinda vituoni hapo,” alisema Amina Suleiman, mkazi wa Sinza-Mori jijini Dar.
Aidha, kwa upande wa waandikishaji nao wamelalamikia wananchi kwa kutozingatia taarifa zinazotelewa juu ya changamoto za kwenda kujiandikisha wakiwa wamejipaka mafuta mikononi hatua inayosababisha mashine kutofanya kazi vizuri.
Waandikishaji hao pia wamezungumzia suala la wananchi kutokuwa wavumilivu katika changamoto hizo wanazokutana nazo pindi wanapokwenda kujiandikisha, hasa pale wanapotumia lugha za kuudhi na kuwataka kuwa wavumilivu