Friday, October 17, 2014

AFYA:MANUFAA YA KABICHI KIAFYA...SOMA HAPA KUFAHAMU


Kabichi ni zao linalolimwa mahala pengi sana hapa duniani. Mboga hii imekuwa ikiwekwa katika hadhi ya chini katika mboga, na hata watu huitumia pale tu wanapoona hakuna jinsi ya kupata mboga ya aina nyingine. Na hivyo utaona ikitumika katika sehemu za jumuiya kama vile shule, magerezani na vyuoni kwani gharama yake ni ndogo hivyo huweza kuhimili hali ya kuinunua kwa matumizi ya watu wengi. Mboga hii ina manufaa mengi sana mwilini lakini iwe ni mpya ya kijani/nyekundu au hata zambarau na siyo ile iliyokaa sana sokoni hadi kusinyaa, hiyo haina manufaa. Mboga hii ina faida zifuatazo:

1. AHUENI YA VIDONDA VYA TUMBO

2. HUIMARISHA MFUMO WA MOYO

3. KINGA DHIDI YA SARATANI

4. INAUPA MWILI VITAMINI VIFUATAVYO:

Vitamin K, Vitamin B12, Vitamin B2, Vitamin A na Vitamin C. Aidha, kabichi ina kiasi kingi cha kambalishe (fiber) Manganizi (Manganese), Potashiamu (Potassium) na Fatty-3 acids. Vyote hivi ni kinga ya mwili dhidi ya magonjwa nyemelezi.