Showing posts with label UDAKU. Show all posts
Showing posts with label UDAKU. Show all posts

Sunday, June 19, 2016

Ommy Dimpoz: "Ndoa ya Mwana FA Haikuwa ya Kifahari Lakini Bora Kuliko Nyingi Nilizowahi Kuhudhuria"

Ndoa ya Mwana FA haikuwa ya kifahari lakini ilikuwa bora, yenye furaha na iliyochangamka kuliko nyingi nilizowahi kuhudhuria, Ommy Dimpoz.

Akizungumza kwenye documentary yangu maalum niliyoipa jina ‘Bado Nipo Nipo ilivyogeuka kuwa historia kwa Mwana FA’, Ommy amedai kujifunza mengi kupitia ndoa ya swahiba wake huyo. 

FA alifunga ndoa June 5, 2016 na mchumba wake wa miaka mingi ambaye tayari pamoja wana mtoto wa kike aitwaye Maleeka.

“Watu wengi wanaogopa kuoa kwasababu ya kufikiria gharama, naweza kusema kwamba ndoa ya Mwana FA haikuwa ndoa yenye mambo ya kifahari lakini ilikuwa moja ya ndoa nzuri kabisa nilizowahi kuhudhuria,” anasema Ommy.

“Haikuwa na mambo mengi kwa maana ya magharama, tumetoka msikitini tumeenda moja kwa moja nyumbani kwake. Baada ya hapo nyumbani kulikuwa tu na kasherehe kadogo tumekusanyika washkaji, kama house party. Ukiangalia kwasababu ilikuwa ndoa ya staa ikawa kubwa,” ameongeza.

Ommy pia amedai kuwa FA alikuwa amepanga kuifanya ndoa itakayohusisha watu wachache sana na ya faragha.
“Mwenyewe alitaka kwamba harusi iwe ni ya watu wasiozidi kumi,” anasema. 

“Hakutaka watu watu wajue kabisa. Tulikubaliana kwamba hakutakuwa na picha hata moja. Kwahiyo mimi nilikuwa nahisi naenda kwenye harusi ambayo sitapost chochote. Lakini nafika msikitini naona watu wako busy wanairekodi Snapchat… nikaona hapa hamna siri na mimi nikaanza kurekodi hapo hapo nikaanza kuzirusha.”

“Baada ya hapo unajua tena ndoa jambo la heri, sio jambo la siri.”

Dokta Atoboa Siri 8 Mimba za Wema Sepetu Kuyeyuka

Imevuja! Kuyeyuka au kuharibika kwa ule ujauzito wa Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu ‘Madam’ hivi karibuni kumetajwa na daktari kuwa ni matokeo ya tabia yake ya kukaidi ushauri wa kitaalam, Amani lina cha kuwapa wasomaji wake.

Hayo yalisemwa na mtu wa karibu we Wema (jina lipo) akizungumzia  masharti ambayo daktari aliyepata kumtibu mrembo huyo aliyasema. Lakini pia, daktari mwingine wa jijini Dar, Dk. Fadhili Emily naye ameibuka na kuliambia Amani kuwa, Wema ana sababu 8 za mimba zake kuyeyuka akiwa anajua au hajui.

DAKTARI WA KWANZA
Mtu huyo wa karibu na Wema alisema mimba ambayo staa huyo aliifanyia shoo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii na kuyeyuka Februari, mwaka huu, ilitokana na sababu ya kugoma kutii masharti ya kitabibu.

SABABU YA KWANZA
“Vipimo vya kitabibu vilisema kuwa Wema alitakiwa kupumzika kwa muda mrefu ili kuilinda mimba hiyo kwani ilikuwa katika hatihati ya kutoka kama mhusika atakuwa ni mzururaji. Sasa Wema akiwa mjamzito alikuwa hakosi viwanja.”

USHAHIDI
Februari, mwaka huu, akiwa mjamzito, Wema alihudhuria tukio la uzinduzi wa Video ya Lupela iliyozinduliwa na Alikiba Salehe kwenye Hoteli ya Slipway, Oysterbay jijini Dar.

SABABU YA PILI
“Ilifika wakati, Wema alitakiwa kupewa bed rest (mapumziko ya kitandani) ili kulinda mimba yake. Hilo nalo likawa gumu kwake kukubaliana nalo. Ndiyo ikawa sababu ya mimba kutoka.”

SABABU YA TATU
“Sababu ya tatu, aliambiwa na daktari wake asifanye kazi ngumu, jambo ambalo lilikuwa likimshinda. Yeye si mtu wa kukubali kukaa tu muda wote. Hilo nalo lilichangia.”
Wema SepetuWema akiwa na mama yake mzazi

SABABU NYINGINE 5
Naye Dk. Fadhili, akizungumza na gazeti hili Jumatatu iliyopita, alisema sababu tatu ambazo zinadaiwa zilichangia mimba ya Wema kuyeyuka ni za kweli, lakini akasema Wema bila kujijua au akijua, mimba zake kadhaa zimeshatoka kwa vile wanawake wengi wenye matatizo ya kutoshika mimba, hushika na kutoka bila wenyewe  kujijua na pia akaanika sababu za hali hiyo kumtokea mwanamke.

Lakini akasisitiza kuwa kuharibika kwa mimba ni tatizo ambalo linaweza kumkumba mwanamke yeyote, si Wema tu.

SABABU ZA KIMAUMBILE
“Sababu za mimba kutoka zenyewe zinatajwa kwamba ni tabia ya kurithi, yaani vinasaba ambavyo si vya kawaida. Kwa hiyo, kiumbe kinakuwa katika hali ambayo kwa asili mimba haiwezi kukua.  Kama mtoto akizaliwa basi atakuwa na matatizo ya kimaumbile na kiakili.”

SABABU YA MUUNGANO
“Sababu nyingine ni kukosekana kwa yai lililorutubishwa.  Katika kuumba, yai la mwanamke hukutana na mbegu ya mwanaume na zoezi la kiumbe kukua huanzia hapo kwa yai kujitenga mara mbili.  Upande mmoja hutengeneza kondo la nyuma na kifuko cha kutunza maji na sehemu ya pili hutengeneza kiumbe au mtoto.

“Huwa inatokea sehemu ya kondo la nyuma inaendelea kukua wakati sehemu ya mtoto haikui. Katika hali kama hii, kama mama hajafanya vipimo kujua maendeleo ya mtoto, uwezekano wa mimba kutoka kabla ya kufikisha wiki 24 ni mkubwa.

“Lakini hili la muunganiko nasema pia kwamba, kwa mwanamke ambaye mimba yake inahofiwa kutoka, ni hatari kuendelea kukutana kimwili na mwanaume wake kwani uwezekano wa kutoka ni mkubwa.”

KUHUSU IDRIS
Hakuna ushahidi wa moja kwa moja kwamba walikuwa wakiendelea ‘kukutana’, lakini kipindi cha ujauzito wake, Wema na Mbig Brother, Idris Sultan uhusiano wao ulikuwa umekolea.

SABABU YA POMBE
“Sababu nyingine inayochangia kuharibika kwa mimba ni unywaji wa pombe kupita kiasi kwa mama mjamzito au kuvuta sana sigara,” alisema dokta huyo.

SABABU YA MAGONJWA
Sababu nyingine alizitaja kuwa ni magonjwa yanayoshambulia mwili wa mama na kiumbe wake tumboni kama vile malaria na kaswende.

SABABU YA KUTOA MIMBA
Daktari huyo alisema kuwa, mwanamke kutoa mimba mara kwa mara kunachangia kuharibika au kushindwa kunasa mimba baadaye.

“Lakini si lazima awe anatoa mimba mara kwa mara, mwanamke anaweza kutoa mimba mara moja tu ikiwa katika mazingira ya ukuaji salama. Hilo linaweza kuwa tatizo kubwa la mimba kutoka siku za usoni,” alisema.

USHAHIDI
Katika mahojiano na gazeti damu moja na hili, Risasi Jumatano mwaka jana, Wema alikiri kuwahi kutoa mimba moja tu ya aliyekuwa staa wa filamu za Bongo, marehemu Steven Kanumba.

WEMA ASAKWA
Mpaka juzi Jumanne, gazeti hili lilikuwa limetimiza siku saba za kumsaka Wema kwa ajili ya kupata vielelezo vyake kufuatia madai au maelekezo hayo ya daktari lakini bila mafanikio kwani hapokei simu na hata alipotumiwa ujumbe mfupi, nao hakuujibu

Chanzo:GPL

Video ya Aibu ya Wema Sepetu Yavuja!

 Video ya aibu inayomuonesha msanii maarufu wa filamu Bongo, Wema Sepetu ‘Madam’ akicheza kihasara mbele ya mwanaume imevuja, Risasi Jumamosi linayo kibindoni.

‘Klipu’ hiyo ambayo Wema anaonekana akikata mauno huku suruali aliyokuwa amevaa ikimvuka na kuacha wazi sehemu ya makalio yake, ilivujishwa hivi karibuni na mdau mmoja wa burudani ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.

“Hii video niliichukua siku ya ile eventi ya Christian Bella ya kutimiza miaka 10 pale Escape One. Wakati akicheza na msanii wa Kundi la Pah One aitwaye Igwe, Wema alionekana kama alikuwa amelewa, alikuwa akikata mauno lakini aibu zaidi ilikuwa pale ambapo ile suruali yake ilipomvuka na sehemu ya makalio yake kubaki wazi.


“Sidhani kama alikuwa kavaa kufuli, baadhi ya watu waliokuwa wakimkodolea macho walishindwa kuamini kama ni Wema yule wanayemjua,” alisema mnyetishaji huyo.
Baada ya mwandishi wetu kupata nafasi ya kuiangalia mwanzo mpaka mwisho, alijiridhisha kuwa aliyekuwa akionekana kwenye video hiyo ni Wema na kweli alichokuwa akifanya ni aibu tupu.

Aibu yake ni pale ambapo suruali inamvuka na kuacha sehemu zake za siri wazi lakini pia staili ya kumkatikia msanii aliyekuwa akicheza naye kwani jamaa alikuwa ‘akikamatia chini’ huku naye akionekana kutokwa na udenda.

Paparazi wetu alijaribu kumtafuta Wema ili kuizungumzia ‘klipu’ hiyo lakini simu yake kila ilipopigwa ilikuwa haipokelewi.

Chanzo:GPL

Utameza Mate Kama Fisi! See What This Naughty Swahili LADY was Doing in Private (VIDEO)

Forget about Wadada wa Mjini and their fake dancing styles, Swahili ladies are the real deal.
They have mastered the skills of teasing men with seductive dance moves that leave little to one’s imagination.

See what this hot Swahili lady was doing in her house. 

Irene Uwoya na Skendo ya Kubakwa!

Untold story! Skendo ambayo haijawahi kuandikwa wala kusimuliwa popote inayomhusu mwigizaji ‘hot’ wa sinema za Kibongo, Irene Pancras Uwoya ‘Mama Krish’ ni juu ya madai ya kubakwa na mfanyabiashara maarufu wa Kihindi jijini Dar (jina linahifadhiwa kwa sasa), alipokuwa na umri wa miaka 18 ambapo kwa sasa ana umri wa miaka 28, Ijumaa limefukunyua na kuinyaka.

Chanzo chetu makini ambacho ni mtu wa karibu wa Uwoya kilichoomba hifadhi ya jina gazetini kilidai kuwa, tukio hilo limekuwa likimtesa Uwoya kwenye maisha yake kiasi kwamba kila akilikumbuka huwa anakosa amani.

KISIKIE CHANZO
“Irene (Uwoya) ana kitu ambacho kinamtesa sana na mara kadhaa amekuwa akiniambia kuwa, ipo siku atakitengenezea filamu, anazungukazunguka sana ila alimdokeza mtu kuwa aliwahi kunusurika kubakwa, labda mkijaribu kumdodosa anaweza kuwapa ukweli,” kilifunguka chanzo hicho na kuongeza:

“Chondechonde asijue tu kwamba mimi ndiye nimewaambia maana alisema skendo hiyo ikiandikwa magazetini na dunia ikajua kilichompata, anaweza akajifungia ndani mwaka mzima kwa aibu.”

UWOYA ANASEMAJE?
Baada ya kuinasa habari hiyo, Ijumaa lilifanya jitihada za makusudi za kumsaka mlimbwende huyo aliyeshiriki Shindano la Miss Tanzania 2006/07 na kushika nafasi ya tano ambapo baada ya kubanwa ipasavyo kwa kuwa alikuwa hataki kusikia habari hiyo, alikiri kunusa skendo hiyo ila akafafanua kuwa, si kweli kwamba alibakwa bali ilibaki ‘kiduchu’ kitendo hicho kikamilike.

“Nikiri tu kwamba ni tukio ambalo sijawahi kulisimulia popote lakini kwa kuwa umenibana, ngoja niseme kilichotokea ili iwe fundisho kwa wengine,” alisema Uwoya na kuendelea:

“Sikumbuki ilikuwa mwaka gani ila ni kweli nilikuwa na kama miaka 18. Nilikuwa na tabia ya kwenda na wenzangu kwenye nyumba ya mfanyabiashara mmoja ambaye alikuwa jirani yetu, Mbezi- Beach (naomba nisimtaje) kuangalia muvi.

“Siku moja, tukiwa kwenye sebule ya tajiri huyo ambaye ana asili ya Kihindi aliyekuwa akiishi peke yake, aliniita chumbani kwake.

“Kwa kuwa tulikuwa tumezoeana sana, sikuwa na wasiwasi wala kudhani angeweza kunifanyia jambo baya. Hee! Ile kuingia ndani si akafunga mlango, wenzangu kule sebuleni hawakujua chochote. Alichokifanya ni kunilazimisha kufanya naye mapenzi kwa nguvu, akaanza kunivua nguo, nikaona hapa nimekwisha.

“Nilichokifanya nilipiga kelele huku nikipiga ule mlango ndipo wale wenzangu walipokuja na kutaka mlango ufunguliwe, jamaa alipoona kimenuka alifungua mlango akatoka nduki na kutokomea nje.”

TAARIFA YAFIKA KWA WAZAZI
Kufuatia tukio hilo, Uwoya alifikisha taarifa kwa wazazi wake ambapo baba yake, Mzee Pancras Uwoya alilivalia njuga na kumfungulia kesi mfanyabiashara huyo, kesi ambayo ilinguruma kwa muda mrefu.

“Ni tukio ambalo liliwashangaza wengi na sikumbuki hasa kilichoendelea ila ninachojua yule mfanyabiashara alitoa fedha nyingi kwa kitendo kile cha kunidhalilisha,” alifunguka Uwoya.

ANAFICHA KUBAKWA?
Alipobanwa juu ya madai kuwa alibakwa ila hataki watu wajue kuwa alifanyiwa kitendo hicho, Uwoya alisema: “Kwa kweli hakufanikisha azma yake, alilazimisha kunivua nguo kweli lakini hakufanikiwa baada ya mimi kupiga kelele.

KWA NINI AMEFUNGUKA LEO?
“Nimeamua kuliweka wazi kwa kuwa umenibana juu ya ishu hiyo na ili watu wajue kwamba sijawahi kukwaa skendo ya kubakwa ‘pasee’ ila nilinusurika kubakwa. Lakini pia nimefanya hivi ili kuwapa fundisho wasichana wengine kutomuamini kila mtu, kwani aliyetaka kunifanyia kitendo hicho ni mtu ambaye sikumdhania.”

Ray C apelekwa sober house Bagamoyo, uongozi wa sober wazungumzia


Muimbaji mkongwe wa muziki nchini, Rehema Chalamila ‘Ray C’ Ijumaa hii amepelekwa Life and Hope & Rehabilitation Centre (Sober House) iliyopo Bagamoyo kwa ajili ya kusaidiwa kuanacha na matumizi ya Madawa ya kulevya, uongozi wa sober hiyo umethibitisha.

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja toka aonekane katika video iliyosambaa katika mitandao ya kijamii ikionyesha jinsi anavyosaidiwa na jeshi la polisi baada ya kudaiwa kutaka kijichoma kisu.

Mmoja kati ya wasimamizi wa kituo cha Life and Hope & Rehabilitation Centre (Sober House) ambacho pia kilimsaidia Chidi Benz kuachana na matuzi ya Madawa ya kulevya, Karim Banji, amesema kuwa ni siku moja toka Ray C apelekwe katika kituo hicho.

“Kweli jana tumempokea Ray C, na kusema kweli kwa sasa siwezi zungumzia maendeleo yake kwa sababu ni siku ya kwanza, lakini leo mchana amekula vizuri na nimemuacha amepumzika,” alisema Karim.

Pia alisema bado hajajua Ray C atakaa kwa muda gani ndani ya sober house.

“Kusema kweli mgonjwa akiletwa hapa, atapimwa afya na baada ya hapo anawekwa katika chumba maalum kwa siku tatu ili aweze kukabiliana na hali ngumu, na baada ya hapo ataendelea na matibabu ya kawaida, kwa hiyo kikubwa ni kuombea tu,” alisema Karim.

Monday, June 13, 2016

PICHA:Msami kafanyiwa suprise na Meneja wake… kapewa gari

Ni mwimbaji na dancer kwenye muziki wa bongofleva anaitwa Msami Giovani leo June 11, 2016 bila kujua kitachotokea baada ya kufanya mazoezi asubuhi, meneja wake aitwae Rehema amemfanyia suprise ya kumzawadia gari aina ya Toyota Ipsum yenye thamani ya Tsh. milioni 15.
Hii ni baada ya single yake iitwayo Mabawa kufanya vizuri kwenye Radio, TV na hata kumpa mauzo ya shows nyingi zaidi majukwaani Tanzania, usisahau kwamba Msami ni bingwa wa kumiliki stage pia.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Mwigizaji Kajala ni miongoni mwa waliokuwepo kwenye suprise
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Meneja Rehema na uthibitisho wa kadi ya gari

Mneno haya RUBY Nna ASLAY yanayotambusha kuwa na mahusiano ya KIMAPENZI

Kama wewe ni mmoja wa watu wanaotumia mitandao ya kijamii hususani instagram, najua huenda ukawa umekutana na post za mastaa wa Bongofleva Ruby na Aslay ambazo zinatafsirika kama wapo kwenye mahusiano. Haijajulikana kwa mara moja kama ni kiki au ni serious ni wapenzi ila hii ndio ishu inayo trend kwa sasa.
rui
asa 2
Aslay baada ya kupata mtoto na majukumu yake mapya ya Umeneja.

Exclusive: Wastara Juma Anasa Ujauzito.......

Exclusive! Habari mpya ya motomoto ni kwamba, staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma amenasa ujauzito, Risasi Jumamosi linakuwa la kwanza kukupa mchapo huu!
Ujauzito huo ni wa aliyekuwa mumewe, Sadifa Juma, mbunge wa Jimbo la Donge, Visiwani Zanzibar ambapo kitendo cha mimba hiyo kuwa ya mbunge, kimemsumbua Wastara hadi kuamua kuondoka ili akapate muda mzuri wa kutafakari nchini Msumbiji.

Taarifa kutoka kwa vyanzo, zinaeleza kuwa Wastara alipoondoka nchini, aliwaaga baadhi ya mastaa wenzake kuwa anakwenda kufuata biashara zake za nguo nchini humo lakini Risasi Jumamosi lilichimba na kupata ubuyu ulionyooka kuwa aliondoka nchini kwa ajili ya kwenda kutafakari ujauzito huo.

NDUGU AVUJISHA UBUYU KAMILI
Ndugu wa karibu na Wastara ambaye hakupenda jina lake lichorwe gazeti, amefunguka kuwa baada ya Wastara kuachika, aligundua ni mjamzito hivyo alichanganyikiwa na kuamua kwenda Msumbiji kwa ajili ya kutafakari zaidi ujauzito huo.
“Hakuwa na jinsi kwani akiangalia alishatoka kwa mwanaume, angewezaje kumwambia kuwa ana ujauzito wake? Akaamua kukimbilia huko kwa ajili ya kujipanga ingawa anavyoonekana anatamani amzalie mbunge huyo,” alisema ndugu huyo.

NDUGU AZIDI KUTIRIRIKA
Ndugu huyo alizidi kushusha ‘vesi’ kuwa mimba ya Wastara inasadikiwa kuwa na miezi miwili au mitatu kwani tangu aachane na mumewe huyo, alikuwa akiumwaumwa na wakati mwingine alikuwa akitapika hovyo ambapo mwanzo alificha lakini yalipomfika shingoni alifunguka.
“Alitufichaficha lakini baadaye akawa hana jinsi, akaona atueleze na sisi tumemshauri tu aende akapumzike na ajiandae kutuletea kiumbe kipya,” alisema ndugu huyo.
Baada ya habari hiyo kutua Risasi Jumamosi,  Wastara alitafutwa kwa njia ya simu ya mkononi, akafunguka:

“Dah! Sijui niseme nini, kiukweli watu wanaongea sana, nimeondoka nchini kwa shughuli zangu binafsi lakini maneno ni mengi, wewe si wa kwanza kunipigia simu. Sikutaka kuongea kabisa juu ya masuala yangu ya ndoa iliyopita wala maisha yangu kwa jumla.”

Risasi Jumamosi: Kwa nini unaongea hivyo wewe funguka swali nililokuuliza, una ujauzito au la?
Wastara: Ndiyo, kwani cha ajabu ni nini? Yule niliyekuwa nalala naye si shangazi yangu, kila mtu anajua niliolewa na aliyenioa (Sadifa) wala si mjomba wangu.

TUJIKUMBUSHE
Wastara aliachika Aprili, mwaka huu baada ya kufunga ndoa na Mbunge wa Jimbo la Donge, Sadifa Juma ambapo ndoa yao ilidumu kwa muda kwa miezi mitatu tu na kuvunjika.

GPL

Video ya wimbo ‘Jike Shuka’ ya Nuh Mziwanda yamtoa povu Shilole..Adai Nuhu ni Mshamba Asiyejua Hata Kubadilisha Boxer

Ikiwa ni siku chache toka Ex wa Shilole, Nuh Mziwanda aachie video ya wimbo ‘Jike Shupa’ ambayo inaelezea jinsi alivyoishi na mpenzi wake huyo, Shilole ameonyesha kukasirishwa na kazi hiyo.

Nuh amethibitisha kwamba Shilole ndiye aliyemuimbia kwenye wimbo huo, kwa kumtumia video queen anayefanana na Shilole kama pacha katika video ya wimbo huo.



Sholole baada ya kuona video hiyo, aliandika ujumbe instagram ambao baadae aliutoa:

"Wale unaongozana nao wanaweza kuwa mizigo au Baraka. Shukrani za dhati kwani kwenye mashabiki zangu ambao ni baraka na pole sana wasanii wote mnaodhani bado tupo dhama za kutumia mgongo wa mtu mwingine kuweza kutoboa. Kipaji siyo maneno ila ni vitengo. Umemiss mkong’oto?. Sipendagi mwanaume mjinga ndiyo maana umekula mkong’oto wa kutosha… Mshamba usiyejua hata kubadilisha boxer, niweke mbali na maisha yako. Nikifungua mdomo wangu utadhalilika....." Shilole

Shilole na Nuh Mziwanda waliachana miezi kadhaa iliyopita ambapo Nuh amekuwa alizungumzia mengi yaliyomkuta wakati akiwa kwenye mahusiano na mwanadada huyo, huku Shilole akitaa kuzungumzia kilichotokea.

Tuesday, June 7, 2016

Shishi Baby Amlia Mingo Raymond wa WCB..Wanaswa Kona Wakipeana Denda...

Meneja wa WCB alisema ''Wasanii wa WCB wanapenda wanawake waliowazid umri kwasababu...)

Yule Ngapepe Sukari ya vijana aka Mario ajulikane kama Shishi Baby juzi kwenye party ya kumkaribisha Rich Mavoko kwenye Lebo kubwa ya Muziki Tanzania WCB alionekana kagandana na kijana mdogo Rayvan mzee wa hapa kwetu huku wakipeana milenda milenda ndimi nje bila kujali watu waliopo.

Sasa sijui ilikuwa ni furaha, pombe, mapenzi au ndio mambo ya kiki!!

Kila laheri kijana.

Faiza Ally: Sipo tayari kurudiana na ‘Sugu’ ila akihitaji mtoto mwingine nipo tayari ‘kumpatia’


Muigizaji na mrembo Bongo, Faiza Ally amesema hayupo tayari kurudiana kimapenzi na baba watoto wake ambaye ni Mbunge wa Mbeya mjini Joseph ‘Sugu’ Mbilinyi, ila yupo tayari kuzaa nae mtoto wa pili.

Akiongea kupitia kipindi cha Kubamba cha Times Fm Jana, bidada huyo Mama wa mtoto mmoja aitwae Sasha amedai hamkumbuki Sugu kwa kuwa hakuwa ‘Romantic’ na alizo nazo kwake ni hisia tu za kupata mtoto wa pili na yeye.

“Sitaki kuzaa na kila Mwanaume, nieleweke wazi sitaki kurudiana na Sugu ila akinifata akidai anataka tuzae mtoto wa pili nipo tayari” Alisema.

Katika ‘line’ nyingine Mama Sasha alisema anajutia kitendo chake cha kutokutumia kinga alipojamiiana na Baba mtoto wake huyo kitendo ambacho kilisababisha kupata Ujauzito.

Diamond: Nadhani Wema Sepetu ameanza kunikubali kimya kimya

Akiwa kwenye kipindi cha Friday Night Live cha EATV, Diamond Platnuzm amesema kitendo alichofanya Wema kupost kazi zake anadhani Wema Sepetu ameanza kumkubali kimya kimya na ameona labda hakuna sababu yeye kuendelea kumchukia Diamond Platnumz, ndiyo maana ameonyesha upendo kwa kusupport kazi zake na za wasanii kutoka kwenye Label yake.

“Kuna wakati inafika watu mnakuwa mmekuwa labda, mtu anaona hana sababu ya kuendelea kukuchukia au kuwa na vita na wewe, sababu mwanzo mwanzo mkiwa bado mnaenda mnaona kuna vitu mko navyo ndiyo maana kuna kuwa na chuki kubwa, lakini ikifika wakati kila mtu amesonga mbele na maisha yake, ameridhika na maisha yake anaona kwanini nimuwekee vita mtu fulani.
Hivyo nadhani labda wakati huo ndiyo huu maana mwenyewe nimeona kweli amepost BET, amepost promo ya Rich Mavoko kwangu mimi nafurahi kwa sababu naona haina faida kwa sisi wasanii kuwekeana vita” alisema Diamond Platnumz.

Mbali na hilo Diamond Platnumz alidai toka ameachana na Wema Sepetu hana namba yake ya simu, hajawahi hata siku moja kumpigia simu wala Wema Sepetu hajawahi kumpigia simu Diamond Platnumz.

Saturday, June 4, 2016

Zari ni Mjamzito tena!!! Mama Nasibu Athibitisha Kwa Maneno haya

Muda si mrefu sana toka Zari na Diamond Platnumz wamepata mtoto wao wa kwanza kwa jina

Kupitia mtandao wa Instagram Mama wa Diamond Platnumz amepost picha ya pamoja akiwa na Diamond Platnumzpamoja na Zari na kuandika "ETI MAMA .K...".


Video: Party iliyofanyika Nyumbani Kwa Diamond Platnumz ya Kumkaribisha Rich Mavoko

June 2 2016 Ndio siku rasmi ambayo Lebel ya WCB ilimtambulisha Rich Mavoko kama msanii wa lebel hiyo, mtu wangu baada ya utambulisho huo uongozi wa WCB uliamua kufanya party ya Kumkaribisha Rich Mavoko pamoja na mke wa Meneja wa Harmonize (Ricardo Momo) kwenye familia hiyo, party ambayo ilifanyika nyumbani kwa Diamond Platnumz

Lulu DivA na Gigy Money Wapeana Makavu Live


WAUZA nyago kwenye video za Kibongo, Lulu Abass ‘Lulu Diva’ na Gift Stanford ‘Gigy Money’ hivi karibuni wamechimbana mikwara na kupakana shombo kila mmoja akimuona mwenzake kituko kutokana na maneno anayoyasikia juu yake.

Ishu nzima ilianza baada ya mwandishi wetu kupata ubuyu kutoka kwa mmoja wa watu wa karibu wa Lulu Diva kuwa anamhofia Gigy Money kumfunika katika gemu wanalofanya.

Baada ya mwandishi wetu kupewa ubuyu huo alimwendea hewani Lulu, aliposomewa  madai hayo mwanadada huyo alisema;

“Nani kakwambia hivyo? Siwezi kumhofia Gigy kwenye kile ninachokifanya, hana kitu chochote cha kunifanya nimhofie maana ni mtu wa kawaida sana kwangu.”

Kwa upande wa Gigy alipotafutwa alisema; “Siwezi kupigizana kelele na huyo demu, anatafuta kiki kupitia kwangu lakini hawezi kuipata hata kwa dawa, haniwezi kwa kila kitu, akajipange sana na akae akijua simuogopi.”

Friday, June 3, 2016

Utapenda alichojibu Wema kuhusiana na katuni hii aliyochorwa na mastaa wengine wenye uhusiano na mastaa wanaowazidi umri

Hivi karibuni gazeti moja la udaku liliwachora mastaa wa kike wenye uhusiano na mastaa wa Bongo wanaowazidi umri. Mastaa hao ni pamoja na Jacqueline Wolper aliyechorwa akimnywesha uji mpenzi wa Harmonize anayeonekana akiwa amebeba mdoli.

Wengine ni Wema Sepetu akiwa amempakata Idris Sultan, Zari the Bosslady akimweka Diamond kwenye kitolori cha kuwafundishia watoto kucheza na Aunty Ezekiel akiwa amembeba mgongoni mpenzi wake Mose Iyobo.

Ni Wema pekee ndiye aliyeijibu kwa kupost picha hiyo kwenye akaunti yake na kuandika: Aliechora hii natamani tu nimuone… Nimpe mkono. Leo nimeongeza siku za kuishi wallahy…. I jus laughed too much today….. Ukisoma na dialogue ndo unakufa kabisa…. Nimeipenda hio ya “Aogopa Mimi… Aogopa chacha.”

Thursday, June 2, 2016

Bifu la Lulu Michael na Hamisa Mobeto Mtandaoni Lasababisha Mange Kimambi Kumlipua Majizo Kuwa ni Muuza Madawa ya Kulevya

Lile bifu linolotikisa kwenye mitandao ya kijamii kwa sasa, linalowahusisha mastaa wenye mvuto wa aina yake bongo, namzungumzia Hamisa mobeto (I phone) na lulu michael (Techno) limefikia mahali pabaya.

Ambapo usiku wa jana mwana mama mwenye vituko vya aina yake aishiye Marekani aitwaye Mange Kimambi amemlipua mwanaume anayedaiwa kuwagombanisha Lulu na staa aitwaye Majizo kuwa ni muuza mada ya kulevya maarufu hapa mjini na ana pesa chafu sana inayowazuzua warembo hao mpaka kufikia hatua ya kuchafuana mitandaoni.

Either mwana mama huyo ameahidi kuanika siri za mwanaume huyo ambaye anasadikika kuwa na utajiri wa kutisha ukilinganisha na umri wake mdogo.

Mange Ameandika haya Katika Ukurasa wake wa Instagram:

mangekimambi_
"Kumbe huyo Majizo mwenyewe ndo wale adui zangu 😡😡😡.Majizo mwenyewe anaepiganiwa na Lulu na Hamisa ni muuza Unga wa Long time. 🙆🏽🙆🏽🙆🏽🙆🏽🙆🏽... Unaambiwa kijana ana pesa chafuuuuuuuuuuuuu Hiyo Efm Kafungua tu ili asafishe hiyo pesa ya Unga, yani unaambiwa ana helaaaaaaaa acha!!! Huyu jamaa alikuwaga ni DJ tu wa Magic FM na Channel Ten taratibu akaanza kujiingiza kwenye biashara ya unga ndo mpaka katajirika na yeye kafungua Redio yake!! . Unaambiwa huo mjumba wake huko Kigamboni ni kufuruuuuuuuuuuu Mengi mwenyewe hana nyumba kama ya huyu kijana, unaambiwa ni balaa. Ila Ndo hivyo mateso ya Kina Ray C Kina Chidi Benzi na vijana wa Kitanzania ndo yanayojenga hayo majumba.Tena nimekuwa warned unaambiwa jamaa mtandao wake ni high level hawezi guswa na mtu hapo Tanzania.... Mtandao wake ni wa vigogo Yani.... 🙆🏽🙆🏽🙆🏽🙆🏽 . Jinsi Maisha yalivyo magumu kuna kijana anaweza Kuwa inspired na story ya Majizo, don't be mwisho wa hawa watu huwa sio mzuri. Siku zooote mwisho wao huwa ni mmbaya. Kulikuwa na muuza Unga tajiri Tanzania kama Shkuba? Jiulize yuko wapi sasa Hivi? Ananyea ndoo mabilioni watu wanayala huko nje, tena bora kipindi cha JK alikuwa anaishi jela kama kwake na mkewe alikuwa anapelekewa every weekend Sasa Hivi ni mfungwa kama wafungwa wengine....😭😭... . . Hivi Magu ile vita ya wauza Unga imeishia wapi???? Mbona ilianza na moto sasa hivi kimyaaaaa?? Watuondelee hawa watu jamani, wanatuulia vijana wetu!! And I'm sure hao Lulu na Hamisa wote wanajua kazi ya bwana yao Ila ndo hivyo wanataka Maisha ya juu so hawajali kuwa wenzao wanakufa, familia zinasambaratika ili tu wao wapendeze na waishi Maisha ya juu😏😏😏😏... Yani nawachukia wauza Unga especially waliotajirika maana it shows wameuwa watu wangapi. Although siamini kuna kitu kama hiko Ila Haki ya Nani for the first time nimewish ingekuwa kweli Lulu awe na jini la kuuwa wanaume ili huyu jamaaa tumpotezee. Wanatumalizia nguvu ya taifa hawa watu. . . Huyu jamaa keshaingia kwenye black list yangu ya wauza Unga.Ntakuwa nawapa habari zake." Mange

Video : Kwa Mtoko Mmoja Wema Sepetu Anavaa Vitu Vyenye Gharama ya Zaidi ya Milioni Mbili

Moja ya kitu kinachomtofautisha mtu maarufu na wakawaida mara nyingi ni kujulikana kwake na mavazi anayovaa. Kwa mfano mzuri tu ni hapa Bongo watu wengi maarufu wamekua wakionekana nadhifu sana kwa kuvaa nguo za gharama.

Kwa mwananchi wa kawaida kununua nguo ya Laki moja ni jambo gumu sana ila kwa star kama Wema Sepetu ni jambo la kawaida sana. Akihojiwa katika EFM Radio Wema Sepetu alifunguka kua kwa kila siku anayotoka vitu anavyovaa gharama yake ni kama milioni 2 za kitanzania.

Hebu msikie kwenye video hii hapa chini..