Thursday, June 2, 2016

Bifu la Lulu Michael na Hamisa Mobeto Mtandaoni Lasababisha Mange Kimambi Kumlipua Majizo Kuwa ni Muuza Madawa ya Kulevya

Lile bifu linolotikisa kwenye mitandao ya kijamii kwa sasa, linalowahusisha mastaa wenye mvuto wa aina yake bongo, namzungumzia Hamisa mobeto (I phone) na lulu michael (Techno) limefikia mahali pabaya.

Ambapo usiku wa jana mwana mama mwenye vituko vya aina yake aishiye Marekani aitwaye Mange Kimambi amemlipua mwanaume anayedaiwa kuwagombanisha Lulu na staa aitwaye Majizo kuwa ni muuza mada ya kulevya maarufu hapa mjini na ana pesa chafu sana inayowazuzua warembo hao mpaka kufikia hatua ya kuchafuana mitandaoni.

Either mwana mama huyo ameahidi kuanika siri za mwanaume huyo ambaye anasadikika kuwa na utajiri wa kutisha ukilinganisha na umri wake mdogo.

Mange Ameandika haya Katika Ukurasa wake wa Instagram:

mangekimambi_
"Kumbe huyo Majizo mwenyewe ndo wale adui zangu 😡😡😡.Majizo mwenyewe anaepiganiwa na Lulu na Hamisa ni muuza Unga wa Long time. 🙆🏽🙆🏽🙆🏽🙆🏽🙆🏽... Unaambiwa kijana ana pesa chafuuuuuuuuuuuuu Hiyo Efm Kafungua tu ili asafishe hiyo pesa ya Unga, yani unaambiwa ana helaaaaaaaa acha!!! Huyu jamaa alikuwaga ni DJ tu wa Magic FM na Channel Ten taratibu akaanza kujiingiza kwenye biashara ya unga ndo mpaka katajirika na yeye kafungua Redio yake!! . Unaambiwa huo mjumba wake huko Kigamboni ni kufuruuuuuuuuuuu Mengi mwenyewe hana nyumba kama ya huyu kijana, unaambiwa ni balaa. Ila Ndo hivyo mateso ya Kina Ray C Kina Chidi Benzi na vijana wa Kitanzania ndo yanayojenga hayo majumba.Tena nimekuwa warned unaambiwa jamaa mtandao wake ni high level hawezi guswa na mtu hapo Tanzania.... Mtandao wake ni wa vigogo Yani.... 🙆🏽🙆🏽🙆🏽🙆🏽 . Jinsi Maisha yalivyo magumu kuna kijana anaweza Kuwa inspired na story ya Majizo, don't be mwisho wa hawa watu huwa sio mzuri. Siku zooote mwisho wao huwa ni mmbaya. Kulikuwa na muuza Unga tajiri Tanzania kama Shkuba? Jiulize yuko wapi sasa Hivi? Ananyea ndoo mabilioni watu wanayala huko nje, tena bora kipindi cha JK alikuwa anaishi jela kama kwake na mkewe alikuwa anapelekewa every weekend Sasa Hivi ni mfungwa kama wafungwa wengine....😭😭... . . Hivi Magu ile vita ya wauza Unga imeishia wapi???? Mbona ilianza na moto sasa hivi kimyaaaaa?? Watuondelee hawa watu jamani, wanatuulia vijana wetu!! And I'm sure hao Lulu na Hamisa wote wanajua kazi ya bwana yao Ila ndo hivyo wanataka Maisha ya juu so hawajali kuwa wenzao wanakufa, familia zinasambaratika ili tu wao wapendeze na waishi Maisha ya juu😏😏😏😏... Yani nawachukia wauza Unga especially waliotajirika maana it shows wameuwa watu wangapi. Although siamini kuna kitu kama hiko Ila Haki ya Nani for the first time nimewish ingekuwa kweli Lulu awe na jini la kuuwa wanaume ili huyu jamaaa tumpotezee. Wanatumalizia nguvu ya taifa hawa watu. . . Huyu jamaa keshaingia kwenye black list yangu ya wauza Unga.Ntakuwa nawapa habari zake." Mange