Thursday, June 2, 2016

Video : Kwa Mtoko Mmoja Wema Sepetu Anavaa Vitu Vyenye Gharama ya Zaidi ya Milioni Mbili

Moja ya kitu kinachomtofautisha mtu maarufu na wakawaida mara nyingi ni kujulikana kwake na mavazi anayovaa. Kwa mfano mzuri tu ni hapa Bongo watu wengi maarufu wamekua wakionekana nadhifu sana kwa kuvaa nguo za gharama.

Kwa mwananchi wa kawaida kununua nguo ya Laki moja ni jambo gumu sana ila kwa star kama Wema Sepetu ni jambo la kawaida sana. Akihojiwa katika EFM Radio Wema Sepetu alifunguka kua kwa kila siku anayotoka vitu anavyovaa gharama yake ni kama milioni 2 za kitanzania.

Hebu msikie kwenye video hii hapa chini..