WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye amezitaka nchi za Afrika kuhakikisha zinakubali kubadilishana madaraka pale chama kimoja kinaposhindwa kuongoza ili kuepusha nchi kuingia kwenye machafuko.
Aidha, Sumaye alisema ni vyema wataalam wakaongoza nchi kwa kubuni mbinu mbalimbali za kujikwamua kiuchumi.
Sumaye aliyasema hayo jana Jijini hapa wakati akizungumza kwenye kongamano la Nafasi ya Wasomi na Wafanyabiashara Katika Kujenga na Kukuza Uchumi wa Nchi, lililoshorikisha viongozi wa vyama, wafanyabiashara na wasomi wa kada mbalimbali wa Arusha.
Sumaye alisema uongozi ni kubadilishana nafasi na katika nchi za Ulaya kwa mfano, chama kikishindwa kutawala kinakubali lakini kwa nchi za Afrika kuna uroho wa madaraka au ubinafsi.
"Tunataka kuwajengea uwezo wasomi wetu kwa kujiamini na kujipatia fursa za kujikwamua kiuchumi," alisema Sumaye ambaye alikuwa Waziri Mkuu kwa miaka 10 mfululizo kati ya 1995-2005, kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi.
"Ubinafsi tuache, tukishindwa uchaguzi achia ngazi.Mimi niliyasema haya nikiwa CCM na leo hii nipo Chadema nasema unapoang'angania madaraka, aidha unaogopa ukiachia utasababisha machafuko au ubinafsi."
Naye Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, Dk. Vincent Mashinji akifungua kongamano hilo, alisema chama chake kinataka kutengeneza mabepari wa kitanzania ambao watajiongeza wenyewe katika kujiinua kiuchumi.
Alisema Arusha ni mji wa kitalii hivyo ni vyema wafanyabiashara wakatumia fursa zilizopo kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi, na inawezekana Jiji hilo kuwa na fursa nyingine za kibiashara badala ya kutegemea madini ya Tanzanite pekee.
“Hatuna barabara, hatuna madawa hospitalini, hatupati fedha kwa sababu hatupati fedha nyingi kwenye kodi zetu, lakini tungeingiza bangi kwenye mfumo wenye kuruhusiwa na tukaweza kuiwekea mazingira rasmi ya matumizi yake tukauza ndani na nje ya nchi tungeweza kukusanya kodi kwa kiasi kikubwa sana, tungejenga nchi yetu”, alisema Afande Sele.
Pamoja na hayo Afande Sele ameonyesha kushangazwa na kitendo cha serikali kukataza bidhaa hiyo ambayo inajumuishwa kwenye madawa ya kulevya, na kuingiza rizla ambazo hutumika kusokotea bangi.
“Taifa tupige hatua lazima tuachane na vitu flan vyenye unafiki, Tanzania wengi wanasema sivuti bhangi lakini upande wa pili wanavuta, au serikali inasema ina sheria za kuzuia bangi lakini bangi zinalimwa vijijini huko bangi zinauzwa na serikali hii hii ambayo ndio inaingiza rizla bandarini zinalipiwa kodi, lakini zile rizla hazina kazi yoyote katika taifa kama sio kunyongea bangi kwa hiyo serikali inafahamu na viongozi wanafahamu lakini bahati mbaya kuna unafiki”, alisema Afande Sele.
Pamoja na hayo Afande Sele ameonyesha kushangazwa na kitendo cha serikali kukataza bidhaa hiyo ambayo inajumuishwa kwenye madawa ya kulevya, na kuingiza rizla ambazo hutumika kusokotea bangi.
“Taifa tupige hatua lazima tuachane na vitu flan vyenye unafiki, Tanzania wengi wanasema sivuti bhangi lakini upande wa pili wanavuta, au serikali inasema ina sheria za kuzuia bangi lakini bangi zinalimwa vijijini huko bangi zinauzwa na serikali hii hii ambayo ndio inaingiza rizla bandarini zinalipiwa kodi, lakini zile rizla hazina kazi yoyote katika taifa kama sio kunyongea bangi kwa hiyo serikali inafahamu na viongozi wanafahamu lakini bahati mbaya kuna unafiki”, alisema Afande Sele.