Wednesday, February 3, 2016

NEY WA MITEGO: MRISHO MPOTO AKIAMUA KUINGIA KWENYE HIP HOP, HAKUNA WA KUMSHINDA BONGO.

Nay wa mitego
Raper Ney wa Mitego amesema, kwa uwezo wa kutunga mashairi alionao Msanii wa nyimbo za asili Mrisho Mpoto, basi akiamua kuingia na kuanza kufanya muziki wa Hip hop asingekuwa na mpinzani Tanzania.
Ney ameuambia mtandao wa Bongo 5 kuwa, labda Fid q ndio msanii pekee anayeweza kushindana na Mpoto.
“Huyu jamaa nafikiria anaumiza kichwa kiasi gani kuandaa kazi zaye, anatumia akili nyingi sana ndio maana nasema akiingia kwenye muziki wa Hip hop atakuwa hana mpinzani” alisema.
Baba Curtis amewataka pia mashabiki wake kukaa mkao wa kula kwani ataachia kazi mpya hivi karibuni.