Rukia Mabeseni akimsuta shoga yake pamoja na wenzie.
“Shost wangu, huyu mama Mariam huyu aliwahi kumzawadia mwanangu baiskeli katika sherehe yake ya kuzaliwa, nikashukuru na nikajua shoga ninaye.“Cha ajabu juzijuzi hapa alikuwa na sherehe yake, bahati mbaya mimi sikuwa kwenye hali nzuri, nikampelekea zawadi ndogo, hee! Kumbe mwenzangu hajaridhika.
“Si akaanza kunisema vibaya kwa watu, eti kama hali yangu ilikuwa mbaya kwa nini sikusema mapema badala ya kumpelekea matambara, kwa kweli iliniuma sana.“Ndiyo nimeamua kumrudishia zawadi yake ya baiskeli kwa staili hii ili aweke kumbukumbu kuwa alichonifanyia si kitu kizuri,” alisema Rukia.
Wakizidi kumsuta.
Hata hivyo, baada ya Rukia kusikia kuwa wameenda kushitakiwa, walirudi tena ambapo safari hii mama Mariam alikubali yaishe kwa kuomba msamaha. “Ameomba msamaha na amefuta kesi kwa sababu alisema kuwa alighafirika tu, hata hivyo alinipigia simu na kuniambia anaumwa anaomba tuongee yaishe ikibidi tukamuone tumalize tofauti zetu,” alisema Rukia.