BONDIA Francis Cheka jana aliendeleza ubabe kwa kumchapa bondia Kiatchai Singwancha kutoka Thailand katika pambano lililofanyika Ukumbi wa PTA uliopo Viwanja vya maonesho vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Pambano hilo Cheka alilimaliza katika raundi ya nane baada ya kumteua bega mpinzani wake.