MTOTO Jackson Hosea (10) wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi Kiseke iliyoko Ilemela, Mwanza ameunguzwa mwilini kwa kisu na imedaiwa kuwa aliyefanya kitendo hicho cha kinyama ni bibi yake aitwaye Laurencia Athanas.
Taarifa zaidi kutoka chanzo chetu ndani ya jeshi la polisi, kimesema kwa njia ya simu kwamba mtoto huyo alifanyiwa unyama huo Mei 23, mwaka huu siku ya Ijumaa jioni.
“Wakati akitoa maelezo polisi, mtoto huyo alikuwa akitokwa na machozi kufuatia maumivu makali aliyoyapata kwa sababu ya kupoteza kalamu ya shilingi 200,” kilisema chanzo.
KALAMU YA SH 200
Imedaiwa kwamba mwanafunzi huyo mara baada ya kutoka shule alijikuta hana kalamu aliyonunuliwa na bibi yake huyo mzaa mama ambaye wanaishi naye ndipo alipoadhibiwa na kubaki na majeraha makubwa mgongoni na kwa sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Bugando, Mwanza.
Imedaiwa kwamba mwanafunzi huyo mara baada ya kutoka shule alijikuta hana kalamu aliyonunuliwa na bibi yake huyo mzaa mama ambaye wanaishi naye ndipo alipoadhibiwa na kubaki na majeraha makubwa mgongoni na kwa sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Bugando, Mwanza.
MIKONONI MWA POLISI
Polisi mkoani Mwanza walipata habari hizo kutoka kwa walimu na majirani wa mama huyo ndipo walikwenda kumkamata.
“Hivi sasa jeshi la polisi linamshikilia bibi huyo mkazi wa Kiseke, Ilemela kwa tuhuma za kumchoma kwa kisu cha moto mjukuu wake na kumsababishia majereha mbalimbali mwilini,” kilisema chanzo.
Polisi mkoani Mwanza walipata habari hizo kutoka kwa walimu na majirani wa mama huyo ndipo walikwenda kumkamata.
“Hivi sasa jeshi la polisi linamshikilia bibi huyo mkazi wa Kiseke, Ilemela kwa tuhuma za kumchoma kwa kisu cha moto mjukuu wake na kumsababishia majereha mbalimbali mwilini,” kilisema chanzo.
Habari zinasema kuwa mtoto huyo akiwa kituo cha polisi, alisimulia kila kitu kuhusiana na unyama huo na alipoulizwa alipo mama yake mzazi alisema anaishi Nzega.
AFISA MTENDAJI
Afisa mtendaji wa eneo hilo, Bi. Hellen Mcharo amelithibitishia gazeti hili kutokea kwa tukio hilo.
Mcharo alisema: “Tukio hilo liliibuliwa kwa mara ya kwanza Mei 25, 2015 na mwalimu mmoja ninayemfahamu kwa jina moja la Midali.
Afisa mtendaji wa eneo hilo, Bi. Hellen Mcharo amelithibitishia gazeti hili kutokea kwa tukio hilo.
Mcharo alisema: “Tukio hilo liliibuliwa kwa mara ya kwanza Mei 25, 2015 na mwalimu mmoja ninayemfahamu kwa jina moja la Midali.
“Alimuona mtoto akiwa na majeraha ya kuchomwa moto na alipomuuliza alisema aliunguzwa na bibi yake, Mei 23, mwaka huu,” alisema kiongozi huyo.