Friday, March 25, 2016

Mfahamu Mtanzania anayecheza soka Uingereza aliyekuja kuitumikia Taifa Stars (+Video)

Adi Yussuf ni mtanzania anayecheza soka la kulipwa katika klabu ya daraja la piliUingereza kwenye klabu ya Mansfield Town. Adi pia amekulia katika klabu ya Leicester City ila kwa sasa yupo Tanzania kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidi ya Chad wa kuwania kufuzu michuano AFCON 2017 Gabon.
“Ni kweli mwanzo ilikuwa ngumu kwa klabu yangu ya Mansfield Town kuniruhusu nije Tanzania kwa sababu ilikuwa tunahitaji kupandisha timu, ila sasa wameniruhusu nije kuchezea timu yangu ya taifa” >>> Adi Yussuf
Zaidi angalia exclusive interview yake aliyofanya na Amhed Ally mwandishi wa Star Tv

CHANZO CHA STAR TV