Saturday, July 19, 2014

SHILOLE: NTAFUNGA NDOA NA MZIWANDA NIWAFUNGE MIDOMO WANAFIKI..w


Msanii  wa  maigizo  na  muziki  wa  kizazi  cha  leo, Zena  Mohammed  'Shilole'  amekuja  juu  na  kusema  anashangazwa  na  habari  zilizozagaa  mjini  kuwa  yeye  amekataliwa  ukweni....

Akiongea  na  Mpekuzi, Shilole  amesema: "Nashangaa  watu  wanasema  eti  nimekataliwa  ukweni  kisa  umri  wangu  kuwa  mkubwa  kuliko  wa  mwanaume. Ninachokijua  mimi  umri  haujalishi  katika  mapenzi, kikubwa  ni  upendo  wa  kweli  na  kuheshimiana.

"Habari  za  mimi  kukataliwa  ukweni  hazina  ukweli  wowote, na  wala  hakuna  mtu  niliyezungumza  naye  kuhusiana  na  hilo  swala  na  wala  hakuna  ndugu  yeyote  wa  Nuh Mziwanda  aliyeonysha  kutonipenda. 

"Nilipokelewa  kwa  furaha  sana  Ukweni  na  habari  njema  ni  kwamba  hivi  karibuni  mtarajie  kuona  ndoa  ili  wanafiki  tuwafunge  midomo  yao,"  alisema  Shilole