Sunday, July 20, 2014

STEVE NYERERE: NDOTO YANGU NI KUJA KUWA RAIS WA TANZANIA..SOMA ZAIDI


Mwenyekiti  wa  Club  ya  Bongo  Movie  Unity, Steven Mengere  'Steve  Nyerere' ndoto  yake  ni  kuwa  mmoja  wa  viongozi  wa  ngazi  ya  juu  hapa  nchini  ikiwa  ni  pamoja  na  kuwa  Rais  kwani  uwezo  wa  kuwaongoza  watanzania  anao.

Akizungumza msanii huyo  amesema  kuwa  kitendo  cha  kuchaguliwa  kuwa  katibu  kata  ya  Bwawani, Kinondoni  jijini  Dar es  Salaam  kupitia  chama  cha  Mapinduzi  CCM,  ni  mwanzo  mzuri  wa  kuelekea  kutimiza  malengo  yake...

"Hakuna  aliyezaliwa  akitambua  kuwa  siku  moja  anaweza  kuwa  miongoni  mwa  viongozi  wakubwa  katika  nchi  hii, lakini  dalili  za  kuwa  huko  huja  kutokana  na  kuwa  na  malengo  mazuri  na  kujitambua  kama  unaweza  kuwaongoza  watu  wengine," alisema  Steve  Nyerere.


Msanii  huyo  alisema  hakuna  kiongozi  anayeweza  kushika  nyadhifa  za  juu  bila  kuanzia  chini  kama  alivyoanza  yeye  na  ndio  maana  wabunge  wengi  huwa  wanaanzia  chini  na  taratibu  wanakuwa  wanapanda  ngazi  kwa  lengo  la  kuona  uwezo  wao  wa  kuongoza