Friday, July 25, 2014

UKATILI WA AJABU .... MUME AMUUNGUZA VIBAYA MKE WAKE SEHEMU ZA SIRI KWA KIJINGA CHA MOTO..TUNAOMBA RADHI KWA PICHA HIZI


Samahani kwa picha hizo lakini napenda kukufahamisha kuwa huyo mhanga anaitwa Agness Marwa mwenye umri wa miaka 18 mkazi wa kijiji cha Mrito , wilayani Tarime.Alifanyiwa ukatili huo na mume wake aitwae Marwa Chacha mnamo tarehe 13/7/2014, baada ya kukuta Tsh 2,000/= kwenye pochi ya mhanga.


Baada ya kumtuhumu kuwa amepewa fedha hizo na wanaume, ndipo akaamua kumpiga na kumfunga kamba na kumweka nje wakati mvua inanyeesha, kama hiyo haitoshi akaaenda jikoni na kuchukua kiginga cha moto na kuanza kumuunguza kama picha zinavyoonesha
Mutuhumiwa ametoroka, na mhanga kwa mila za kikurya alificha hilo tukio hadi tarehe 17/7/2014 ndipo akapelekwa hospitali ya Sungusungu iliyoko Nyamongo.
Kamanda wa polisi kanda maalumu anasema mtuhumiwa pamoja na mama yake wametoroka na hii ni baada ya kuchelewa kutoa taarifa ,hata hivyo jeshi la polisi linaendelea kufanya upelelezi ili waweze kumkamata mthumiwa na kumpeleka kwenye vyombo vyenye Mamlaka.
Shirika la sheria na haki za binadamu Tarime(SHEHABITA) linaendelea kufuatilia tukio hili kwa karibu na kutoa rai kwa wananchi kuacha kufanya ukatili dhidi ya wanawake na watoto

TIZAMA PICHA JINSI ALIVYOUNGUZWA.....PLEASE NASISITIZA PICHA SIO NZURI KABISA..18++
>>PICHA YA KWANZA<<

>>PICHA YA PILI<<
>>PICHA YA TATU<<