KOCHA Louis van Gaala amewasili na kikosi chake cha Manchester United mjini Las Vegas, Marekani na kwenda ufukwe wa Santa Monica katika ziara yao ya kujiandaa na msimu.
Mholanzi huyo na kikosi chake cha nguvu cha wachezaji 25 walitua Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Los Angeles jana na moja kwa moja kwena ufukwe huo.
Wachezaji wa United walivalia suit nyeusi nadhifu na walionekana wamependeza wakati wakienda ufukwe huo ambako wamefikia katika hotel ya Beverly Hills watakapolala kwa siku sita.
Wanawasili: Wachezaji wa Manchester United wakiteremka kwenye ndege baada ya kuwasili Los Angeles
Kocha mpya wa Manchester United, akitaniana na mshambuliaji Wayne Rooney Uwanja wa Ndege
Mchezaji mpya Ander Herrera akisaini autographs za mashabiki
ZIARA YA MANCHESTER UNITED KUJIANDAA NA MSIMU 2014
Mashetani hao Wekundu watacheza mechi nne Marekani, wakianza na timu ya zamani ya David Beckham.
Kombe la Chevrolet
LA GALAXY in Los Angeles, Julai 23
Kombe la Kimataifa
AS Roma in Denver, Julai 26
Inter Milan in Washington DC, Julai 29
Real Madrid in Ann Arbor, Agosti 2
KIKOSI CHA MANCHESTER UNITED ZIARANI
De Gea, Lindegaard, Amos, Johnstone, Rafael, Evans, Smalling, Jones, Shaw, Blackett, M Keane, James, Herrera, Cleverley, Fletcher, Young, Zaha, Kagawa, Mata, Valencia, Nani, Lingard, Welbeck, Rooney, W Keane