Wednesday, July 23, 2014

WEMA APATA GONJWA LA NGOZI..SHAVU LAHARIBIKA VIBAYA..ASHINDA NDANI....UREMBO WOTE KWESHINEY !

MISS Tanzania 2006/07 Wema Sepetu amesema ugonjwa wa ngozi ulioshambulia sehemu ya shavu lake la kushoto umeharibu urembo wake na kumfanya ashindwe kutoka.
Miss Tanzania 2006/07 Wema Sepetu. 
Akizungumza kwa huzuni , Wema alisema hakutegemea kama tatizo hilo lingekuwa kubwa, kwani lilianza kama kipele kidogo ambacho baadaye sehemu kubwa ilivimba na kuharibu mwonekano wake.
“Ulianza muwasho, kikawa kipele kisha kikageuka kama kishilingi.

Nilipokwenda hospitali nilipewa dawa ya crime ya kupaka, mimi nikachua eneo lililoathirika, kumbe ndiyo nikawa nasababisha matatizo, kukavimba zaidi kama unavyoona,” alisema Wema ambaye alikataa kupigwa picha.