Wednesday, November 5, 2014

MAJAMBAZI WAMEVAMIA NYUMBANI KWA HUYU MCHEZAJI MWINGINE WA AFRIKA KUSINI.

sibusiso-vilakaziSiku chache baada ya mazishi ya kipa na nahodha wa timu ya taifa ya Afrika Kusini na klabu ya Orlando Pirates Senzo Meyiwa kuzikwa baada ya kuuwawa na majambazi, mchezaji mwingine wa timu ya taifa ya Afrika kusini amevamiwa na majambazi nyumbani kwake.
Majambazi watatu ambao bado hawajafahamika walivamia nyumba anakoishi kiungo mshambuliaji wa BafanaBafana Sibusiso Vilakazi ambako walipora vitu kadhaa vya thamani.
Kwa mujibu wa ripoti iliyothibitishwa na mchezaji mwenyewe, majambazi hao walivamia nyumba ambamo mchezaji huyo anaishi na wanae na walimuulizia mchezaji huyo kiasi kwamba ikaonekana kabisa walipanga kumdhuru.
sibusiso-vilakazi(2)Hata hivyo wazazi wa Sibusiso waligoma kutaja mahali alipo kitendo kilichofanya majambazi hao kuondoka bila kumdhuru mtu yoyote ambapo wakati mkasa huu ukitokea Vilakazi alikuwa amelala usingizi kwenye nyumba iliyoko hatua chache toka iliko nyumba iliyovamiwa na hakutambua chochote kilichokuwa kinaendelea hadi aliposimuliwa asubuhi yake.
Vilakazi ambaye ni nahodha wa klabu ya Bidvest Wits ameelezea kusikitishwa kwake na tukio hilo hasa ukizingatia kuwa bado hajasahau kilichomkuta mchezaji ambaye alikuwa akilala naye kwenye chumba kimoja kwenye kambi ya timu ya taifa Senzo Meyiwa.