Taswira Wananchi Katika Picha Sehemu Wanapouza Magazeti Katika Jiji la Dar
Wananchi wakiwa wamejazana katika maeneo tofauti ya kuuzia magazeti ili kujua kilichotokea na kitakachotokea kuhusiana na wizi wa shilingi bilioni 306 za Escrow kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
BAADA ya ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kusomwa jana Bungeni, mtandao huu wa Global leo umezunguka sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam, kuona hisia zao kuhusu wizi wa shilingi bilioni 306 uliofanywa na viongozi wa serikali, dini, taasisi mbalimbali.
Kuonyesha kwamba wengi wao walikuwa wanalifuatilia suala hili, ni jinsi walivyovamia meza za uuzaji wa magazeti kwa wingi ili kujua kilichotokea na nini kinatarajiwa kutoke