Tuesday, December 23, 2014

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAKAZI, ANNA TIBAIJUKA AMETENGULIWA RASMI NAFASI YAKE YA UWAZIRI, PROF MUHONGO AWEKWA KIPORO

 Anna Tibaijuka
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Kikwete amemaliza hutuba yake na Wazee wa Jiji la Dar es salaam huku mada kubwa ikiwa ni sakata la Tegeta Escrow na Kumalizia kwa kutoa maamuzi ya Kumuwajibisha waziri wa Ardhi na Makazi, Anna Tibaijuka kwa kutengua wadhifa wake wa UWAZIRI.
Mh. Jakaya Kikwete
Mh rais alisema "Waziri Tibaijuka alifanya makosa kimaadili; tumemwomba AnnaTibaijuka apumzike tumteue mwingine!"

Pia Mh Rais amesema kuwa "Waziri wa Nishati na Madini Prof. Muhongo huyu nimemuweka kwanza kiporo maana bado uchunguzi unafanyika"