Video ikiwaonyesha mateka wa Kijapan, Kenji Goto Jogo na Haruma Yukawa, walio katika nguo za rangi ya chungwa, wakiwa na Jihadi John anayedai fidia ya Dola milioni 200 ili kuwaachia mateka hao.
Wapiganaji wa Taifa la Kiislam (ISIS) wametoa picha za video ambapo wanatishia kuwaua mateka wawili wa Kijapan kama hawatalipwa Dola milioni 200 (Sh. Bilioni 358) katika muda wa saa 72 zijazo.
Tishio hilo limekuja baada ya Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe, kuahidi kutoa kiasi hichohicho cha fedha kama msaada usiokuwa wa kijeshi kwa nchi zinazopigana dhidi ya ISIS.
Video hiyo iliyosambazwa katika tovuti zinazohusiana na wapiganaji hao, zilizomwonyesha mpiganaji mwenye lafudhi ya Kiingereza ambaye anajulikana kama ‘Jihadi John’ aliyeonekana katika video za mauaji ya kuwakata vichwa mateka David Haines, Alan Henning (Waingereza), na James Foley na Steven Sotloff (Wamarekani) hivi karibuni.
BOFYA KIPICHA HAPO CHINI KUONA VIDEO