Vicent Kigosi maarufu kama Ray sio mahili kwenye sinema tu, bali ni mchezaji mzuri wa soka na pia ni shabiki mkubwa wa Yanga. Akifungwa hasa na Simba basi ataandika machungu yake yote kwenye instagram.Ushabiki wake unapata utani wa jadi kutoka kwa rafiki yake JB ambae ni shabiki mkubwa wa Simba.
Baada ya ushindi mnono wa Yanga, Ray hakuficha furaha yake na akaingia instagram ku-post maneno haya huku akim-tag mwenzake JB kwa kumdhihaki.