Thursday, May 7, 2015

YANGA WAKABIDHIWA KOMBE LA UBINGWA NA ZAWADI KUTOKA FIFA, WAANGUSHA PATI SI LA KITOTO TAIFA

Wachezaji na viongozi wa Yanga SC wakifurahia Kombe lao la ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Habari wa Habari Vijana Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga SC walikabidhiwa Kombe hilo baada ya mechi na waliokuwa wanashikilia taji hilo, Azam FC ambayo walifungwa 2-1 na washindi hao wa pili wa msimu huu.  

Sherehe za ubingwa baada ya kukabidhiwa Kombe lao

Waziri Dk Fenella (katikati) akimkabidhi Nahodha wa Yanga SC, Nadir Haroub 'Cannavaro' cheti kutoka Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA). Kushoto ni Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Yanga SC, Yussuf Manji
Dk Fenella akimvalisha Medali Nahodha wa Yanga SC, Cannavaro