Sunday, April 3, 2016

Ronaldo Kasherekea Ushindi Dhidi Ya FC Barcelona Akiwa Na Nguo Ya Ndani Tu

Baada ya uwepo wa tambo za mashabiki wa soka wa pande za Real Madrid na FC Barcelona kwa zaidi ya wiki moja kuhusu mchezo wa marudiano wa EL Clasico, usiku wa April 2 ilikuwa ni zamu ya kupata majibu ya tambo za mashabiki wa pande zote.

Ukiachana na ushabiki, takwimu za karibuni za vilabu hivyo zilikuwa zinaonesha yoyote anaweza akashinda, kwani timu zote mbili mechi zao tano zilizopita kila timu wamepata ushindi, ila katika mechi tano walizocheza dhidi yao FC Barcelona alikuwa kashinda mara tatu na Madrid mara mbili.