Azerbaijan 'walipaki basi' wakicheza na walinzi 10 na Italia ikapata tabu sana kuupenya ukuta wao hadi Chiellini alipotumia makos a ya kipa kuipa Azzurri bao la kuongoza dakika ya 44.
Chiellini akajifunga kuisawazishia Azerbaijan dakika ya 76 katika harakati kuokoa mpira wa kona- lakini bahati nzuri akasahihisha makos a yake kwa kuifungia Italia bao la ushindi dakika ya 82.
katika mechi nyingine za Kundi H, Croatia imeifunga 1-0 Bulgaria bao pekee la Nikolay Bodurov la kujifunga dakika ya 36 na Norway imeifunga 3-0 Malta, mabao ya Moeller Daehli dakika ya 22 na Joshua King dakika ya 26 na 49.