Sunday, September 28, 2014

KIVAZI CHA JOKATE MH NI SHIDAAA CHAWAACHA MIDUME MIDOMO WAZI

MWANAMITINDO na mtangazaji mahiri Bongo, Jokate Mwegelo amezua utata baada ya kupiga picha akiwa ametinga suruali iliyochanika.
Mwanamitindo na mtangazaji mahiri Bongo, Jokate Mwegelo.
Akizungumzia picha hiyo ambayo imevuja katika baadhi ya mitandao, Jokate alisema alivalia mavazi hayo hivi karibuni Afrika Kusini alipokuwa amekwenda kurekodi wimbo wake mpya (hakuutaja jina) na alivaa makusudi ili kuonesha utofauti.
Jokate Mwegelo akipozi na mzungu.
“Nimeamua tu kuwa tofauti maana hata watu wengi walikuwa wakijiuliza kulikoni mimi kuvaa hivyo  lakini mimi nafikiri lazima kuna wakati tunatakiwa kuonekana tofauti na siyo mapambo muda wote ukibadilika hata unachofanya unakuwa tofauti,” alisema Jokate.