Ivo alifanyiwa vipimo nchini Afrika Kusini mapema wiki hii na tiba za kumuondolea maumivu kabisa, ili Jumamosi aweze kufanya kazi iliyomsababisha akasajiliwa Simba SC Desemba mwaka jana kutoka Gor Mahia.
Ivo alihitaji wiki nane za mapumziko baada ya kuumia kidole gumba mwisho mwa mwezi Septemba, lakini kutokana na kuumia kwa kipa wa pili, Hussein Sharrif ‘Cassilas’ amelazimika kufupisha muda wa mapumziko.
![]() |
Kipa Ivo Mpaunda wakati anafanyiwa vipimo Afrika Kusini |
![]() |
Ivo akiwa anapimwa kidole chake gumba kilichoumia |
Fiziki ya mwili iko sawa kwa Ivo kwa sababu alipoumia kidole alipumzika wiki mbili tu na baada ya hapo akaanza mazoezi ya kukimbia na kujitupa tupa kama anachupia mipira.
Na baada ya tiba ya Madaktari bingwa Afrika Kusini, Ivo amekuwa akisema anajisikia vizuri- maana yake yuko tayari kuwazuilia michomo Yanga SC Jumamosi.
Kipa wa tatu, Peter Manyika aliyedaka mechi tatu baada ya Cassilas kuumia, akimalizia ya sare ya 0-0 na Orlando Pirates, ya kufungwa 4-2 na Bidvest Wits na 2-0 jana na Jomo Cosmos naye anaonekana kuwa vizuri kabisa.
Licha ya umri na uzoefu mdogo, lakini Manyika amejizolea sifa nyingi Afrika Kusini kutokana na udakaji wake mzuri katika mechi hizo tatu za kirafiki.
-BIN ZUBEIRY