Thursday, October 16, 2014

UKATILI! MTOTO MIAKA 16 AMBAKA MTOTO WA DADA YAKE MWENYE MIAKA 3...SOMA ZAIDI

JESHI la Polisi mkoa ni Kilima njaro, linamshikilia kijana mwenye umri wa miaka 16,mkazi wa Sabuko, Wilaya ya Siha ,mkoani humo kwa tuhuma za kumbaka mtoto wa dada yake mwenye umri wa miaka mitatu(wote majina yanahifadhiwa).

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo, Koka Moita, alisema mtuhumiwa anadaiwa kumbaka mtoto huyo nyumbani kwao na kumsababishia maumivu makali sehemu zake za siri.

"Tukio hili limetokea saa 10:45 alasiri,wakati mama wa mtoto huyo akiwa ametoka nyumbani kwenda kwenye shughuli zake za kujitafutia riziki na kumuacha mtoto na mjomba wake ndipo mtuhumiwa alitumia muda huo kufanya kitendo hicho cha kikatil i na kinyama," alisema Kamanda Moita.

Aliongeza kuwa,mama wa mtoto huyo aliporudi nyumbani jioni,alimkuta mtoto wake akilia kutokana na maumivu makali na alipomchunguza akabaini alibakwa.

"Baada ya kubaini mtoto wake amebakwa, alitoa taarifa polisi ambao walimkamata mtuhumiwa na kufikishwa Kituo cha Polisi kwa mahojiano kabla yakufikishwa mahakamani," alisema.

Kamanda Moita alisema kwa sasa mtoto huyo anaendelea na matibabu katika Hospitali ya KibongĂ­to, iliyoko wilayani humo ambapo jeshi hilo linaendelea na uchunguzi.

Alitoa wito kwa wazazi na walezi kuwa waangalifu na watoto wao kutokana na matukio ya ubakaji hususani kwa watoto kuongezeka siku hadi siku.

"Awali matukio ya ubakaji hayakuwepo hapa Kilimanjaro tofauti na sasa...tatizo hili linachangiwa na ukosefu wa maadili kwenye jamii, tabia hii inapaswa kukoma mara moja," alisema.