Thursday, February 5, 2015

Ajali ya ndege Taiwan, wapo waliofariki na majeruhi (Pichaz & Video)

NdegeMpaka Jumatano usiku watu waliokua wamefariki kwenye ajali hii ni 31 huku 12 wakiwa hawajulikani walipo baada Ndege inayoimilikiwa na Shirika la Taiwan la TransAsia kupata ajali na kuangukia kwenye mto katika mji wa Taipei.
Taarifa zinasema kuwa watu 58 walikuwa ndani ya ndege hiyo, huku watu 16 wameokolewa na kupelekwa Hospitali na wengine 10 bado wamenasa katika ndege hiyo ambapo waokoaji wamelazimika kuikata ndege hiyo ili kuwaokoa watu ambao bado wapo ndani.
Picha zinaonyesha ndege hiyo ikiwa imezama kwa kiasi kikubwa katika mto Keelung, ndege hiyo ilipita karibu na magari na kudondoka mtoni muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Songdshan, Taipei kuelekea uwanja wa ndege wa Kinmen nje ya Taiwan huku  chanzo cha ajali  kikiwa bado hakijajulikana.
_80771202_80771155
_80771208_80771207
_80772916_80772915
0

150204005632-taiwan-plane-crash-transasia-more-super-169
images (1)
taiwan-plane-crash