Wednesday, February 18, 2015

SAMATTA APIGA BONGE LA BAO HAJAWAHI TANGU AZALIWE

Kareem Mbwana Samatta amezaliwa
MSHAMBULIAJI wa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokraasia ya Kongo (DRC), Mbwana Ally Samatta ameonyesha yeye si mkali wa mabao uwanjani tu anapokuwa na jezi ya klabu hiyo au timu a taifa ya Tanzania, Taifa Stars, bali hata kitandani anafanya vizuri.

Hiyo inafuatia mchezaji huyo wa zamani wa Mbagala Market, African Lyon na Simba SC kupata mtoto wa kiume aliyempa jina Kareem.

Mtoto huyo amezaliwa Dar es Salaam wiki iliyopita wakati baba yake akiwa kazini, Lubumbashi, yalipo makao makuu ya Tout Puissant Mazembe. 
Mbwana Ally Samatta, ukipenda muite 'Baba Kareem'