Wednesday, April 1, 2015

DIAMOND: NINA UWEZO WA KUFANYA MUZIKI WOWOTE

Staa wa Bongo Fleva,Diamond Platinumz amefunguka kuwa ana uwezo wa kufanya muziki wa aina yoyote kipaji ambacho amejaaliwa na Mwenyezi Mungu.

Hivi karibuni Diamond aliwashangaza mashabiki wake baada ya kuachia wimbo wake mpya kwenye mtandao wa You Tube wenye asili ya mduara uutwao ‘’Nasema Nawe’’ambao amemshirikisha Malkia wa Mipasho,Khadija Kopa. ‘’Namshukuru Mungu amenijalia kipaji kwani nina uwezo wa kufanya muziki wa aina yoyote ule na pia kupitia Video ya wimbo huu nitakuwa nimemfungulia njia producer na Director Hanscana kujulikana Kimataifa,’’alisema Diamond.