Sunday, April 5, 2015

IZZO BIZNESS: BADO SIJAFIKIA UWEZO WA KUFANYA VIDEO YA THAMANI YA MILIONI 40

Izzo Bizness amedai kuwa bado hajafikia uwezo wa kufanya video za thamani kubwa kama baadhi ya wasanii wa Tanzania akiwemo Diamond Platnumz wanavyofanya.


Rapper huyo ambaye wiki hii ameachia video na wimbo mpya uitwao ‘Kidawa’ aliomshirikisha Shaa, amedai kuwa nia ya kwenda kimataifa ipo na anajipanga kufika huko pia.

“Natamani sana kufanya kazi nje ya nchi, kuna watu wametangulia wameenda na wameleta kazi nzuri tunaziona, lakini natamani na mimi nikienda nikirudi watu wasema ‘dah jamaa kwelia alienda,” Izzo ameiambia Kikwetu Blog.

Bado sijaweza mimi kufika bajeti ya kwenda kumlipa mtu milioni 20, milioni 40. Kwasababu baada ya kulipa milioni 20, milioni 40 lazima ujue unafanyaje promotion ya nyimbo yako.

Izzo ameongeza kuwa anapanga na muongozaji wake, Nick Dizzo nao kusafiri kwenda nje ya nchi kufanya video