Wednesday, April 1, 2015

KIMENUKA BUNGENI; WABUNGE WAPIGA KELELE WAKITAKA MAJIBU KURA YA MAONI

Mbunge wa Ubungo (Chadema) akichangia mada bungeni.
SPIKA wa Bunge, Anne Makinda ameamua kulihairisha bunge hadi hapo baadaye baada ya vurugu kuibuka kwa baadhi ya wabunge wakitaka hoja ya kuhairisha mchakato wa kura ya maoni ijadiliwe na kura ya maoni isogezwe mbele maana muda hautoshi.
Spika wa Bunge, Anne Makinda.
Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika alisimama na kusema: "Nimesimama kupata idhini kwa mujibu wa kanuni ili shughuli za bunge zisitishwe badala yake tujadili zoezi la uandikishaji nchi nzima, mpaka sasa zoezi halijakamilika hata kwa mkoa mmoja tu wa Njombe, jambo hili ni la dharura na ilishatolewa na ukaagiza kamati ishughulikie, majibu tupate kikao hiki na leo tunafunga mkutano hamna kitu"
Spika Makinda alijibu: Hoja hii inafanana na ile ya kwanza, nimesema majibu mtajibiwa baadae ndipo wabunge waliposimama na kupiga kelele wakitaka majibu na Spika Anne Makinda akalazimika kusitisha bunge hilo kwa muda.