Ligi kuu ya Uingereza imezidi kusisimua tangu kampeni ya msimu 2014-2015 ianze huku baadhi ya timu zikionyesha viwango vya hali ya juu sana wakati nyingine zikionekana kuhaha.
Baadhi ya wachezaji wamekuwa wakitoa mchango mkubwa sana katika timu zao na kuhakikisha zinapata matokeo yaliyo mazuri kwenye kila mchezo.
Wachezaji ishirini wameingia katika kinyang'anyiro cha kuwania uwanasoka bora wa mwaka wa Ligi hiyo maarufu zaidi duniani ambapo watachujwa na kubakia sita ifikapo mwezi Mei.
Ifuatayo ni orodha ya wachezaji wanaopewa nafasi ya kushinda tuzo ya mchezaji bora wa msimu huu:
# | Mchezaji | Timu |
---|---|---|
1 | Eden Hazard | Chelsea |
2 | Harry Kane | Tottenham Hotspur |
3 | Diego Costa | Chelsea |
4 | Sergio Agüero | Manchester City |
5 | Cesc Fabregas | Chelsea |
6 | Alexis Sanchez | Arsenal |
7 | David de Gea | Manchester United |
8 | Raheem Sterling | Liverpool |
9 | David Silva | Manchester City |
10 | Philippe Coutinho | Liverpool |
11 | Santi Cazorla | Arsenal |
12 | Wayne Rooney | Manchester United |
13 | Thibaut Courtois | Chelsea |
14 | Christian Eriksen | Tottenham Hotspur |
15 | Nemanja Matic | Chelsea |
16 | Yaya Toure | Manchester City |
17 | Chris Smalling | Manchester United |
18 | Daniel Sturridge | Liverpool |
19 | Robin van Persie | Manchester United |
20 | Steven Gerrard | Liverpool |