Friday, June 19, 2015

JACK PATRICK AENDELEZA MITINDO GEREZANI CHINA

Imelda Mtema
Mwanamitindo wa Kibongo, Jacqueline Patrick ameendeleza fani yake ya mitindo akiwa gerezani huko Macau nchini China na kuwa kivutio kikubwa kwa wafungwa wenzake.
Mwanamitindo wa Kibongo, Jacqueline Patrick.
Chanzo chetu ambacho kinadili na masuala ya urembo na mitindo kilisema kuwa, licha ya Jack kuwa gerezani amekuwa akifuatilia mitindo mipya iliyoingia mjini kisha kuwafanyia wenzake.
Chanzo hicho kilisema kazi hiyo imeufanya uongozi wa gereza hilo kummwagia sifa.
Jack anatumikia kifungo cha miaka sita baada ya kukutwa na hatia kutokana na kujihusisha na biashara haramu ya madawa za kulevya.