Wednesday, June 10, 2015

Jose Mourinho Ajisifia Kwanini Huwa Anapaki Bus Uwanjani

Sifa kubwa ya Mourinho na wachezaji wake pale wanapozidiwa uwanjani ni kuweka defence ya wachezaji wengi hadi kupewa sifa ya kupaki bus uwanjani.

Sasa kwenye mkutano na waandishi wa habari Jose aliulizwa kuhusu hiyo sifa mbaya lakini jamaa aliijibu kwa kujisifia kama hivi.

“Kwanza kabisa nina heshima kubwa kwa wandesha mabasi wote, inabidi uwe na skill nzuri sana ili uwe dereva wa bus. Kupaki bus unaitaji kuwa usaidizi lakini kama hauna utaligonga bus lako.”

“Kwenye mpita kuna nyakati tofauti, ni vigumu kuwa na aina moja ya mchezo kuanzia mwanzo wa mechi hadi mwisho. Kuna wakati unatawala mchezo kuna wakati unatawaliwa na mpinzani wako. Mpinzani wako akiwa juu yako kwenye mchezo itabidi ubadilishe mchezo kitu ambacho ni kigumu sana kubadilisha mchezo wakati upo uwanjani.”

“Inaitaji muda mrefu sana kuelewa hiki kitu kwenye mpira, kuna wakati naona vijana wangu wanacheza mpira sana kuliko wachezaji wengine wanaenda uwanjani kujifurahisha au kufurahia mchezo badala ya kucheza. Wakati mwingine ishu sio hiyo, ishu siyo kufurahia mchezo tu bali inabidi ucheze mpira utakaoleta matokeo kwenye timu”

Alimaliza hivyo akisisitiza kwamba wanacheza vile kutokana na mabadiliko yanayotokea mchezoni na lengo lao ni kupata matokeo na sio kucheza tu mpira.