Monday, June 29, 2015

STEVE NYERERE ATANGAZA NIA YA KULIWANIA JIMBO LA KINONDONI

Mwigizaji maarufu Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, akitangaza nia yake ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam, jana kwenye Viwanja vya CCM Kinondoni Bwawani.
Mmoja wa viongozi wa Kata  hiyo akimkaribisha Steve Nyerere kwenye jimbo hilo.
Steve Nyerere akiongea jambo na mmoja wa viongozi wa wanawake waliojitokeza kwenye hafla hiyo.
Msanii wa Filamu, Esher Buheti (kulia), akiwa katika pozi na Lemtuz wakati hafla hiyo ikiendelea.
Wanenguaji wa kike wa Twanga Pepeta wakicheza mbele ya msanii wa filamu JB na wageni wengine waliojitokeza mahali hapo.
Msanii wa Filamu (wa pili kulia),Ikumpa  akicheza na wacheza shoo wa Bendi ya Twanga Pepeta.
Starah Thomas akishirikiana kuimba moja ya wimbo na Bendi ya Twanga Pepeta.
JB akimwaga pesa kwa mmoja wa wapiga gitaa wa bendi hiyo.
 Mama mzazi wa Steve Nyerere akiwa amenyanyua mkono juu wakati mwanaye akimtambulisha kwa wakazi wa Bwawani Kinondoni.
Baadhi ya wasanii wakinyanyua mikono juu kama ishara ya kumuunga mkono Steve Nyerere kwenye mbio zake za kuwania ubunge wa jimbo hilo.
Msanii wa filamu, Ndumbagwe Misayo ‘Thea’ (katikati), akifurahia jambo na wenzake kwenye hafla hiyo.
 
Steve Nyerere akisalimiana na mmoja wa wageni wake.
 
JB akimpongeza Steve Nyerere kwa hatua hiyo.
MCHEZA sinema ambaye pia anakipaji cha kuigiza sauti za watu mbalimbali hapa Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, jana alitanga rasmi adhima yake ya kuliwania Jimbo la Kinondoni katika nafasi ya Ubunge.
Steve aliweka wazi nia yake hiyo jana jioni katika Viwanja vya CCM Kinondoni Bwawani, ambapo watu mbalimbali walijitokeza kumpa sapoti wakiwemo wasanii kadhaa wa Bongo Movies huku Bendi ya Muziki wa Dansi ya The African Stars ‘Twanga Pepeta International’, ikitoa burudani mahali hapo.