Wednesday, June 10, 2015

URAIS KWELI UMEKUWA RAISI,WAKILI MAHAKAMA KUU ATANGAZA KUGOMBEA URAIS 2015

Mwapongo akionyesha fomu ya urais katika viwaja vya Mnazi Mmoja Dar.
Baadhi ya kada wa Chama Cha Mapinduzi na wananchi wakimshangilia.

Taswira ilivyokuwa Mnazi Mmoja.
Mwapongo (kushoto) akiwa na kada wa Chama Cha Mapinduzi (kushoto), kulia ni meneja wake wa kampeni, Lucy Mbutolwe.
Sehemu ya wananchi waliohudhuria hafla hiyo.
Mwapongo akizungumza jambo wakati wa mkutano huo.
WAKILI Mwandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Godwin  Mwapongo,  ametangaza nia ya kuwania urais wa Tanzania mwaka 2015.
Wakili huyo ametangaza nia yake hapo jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam ambapo tayari alikuwa amekwishakuchukua fomu ya urais aliyoionyesha kwa wananchi.
Alisema aliamua hivyo ili kuijengea nchi  misingi imara ya umoja, amani na maadili mema na kupambana na rushwa.
Aliongeza kuwa endapo atateuliwa atahakikisha anapambana na umaskini kuboresha elimu,  afya na  kumwezesha mtu wa kipato cha chini awe na uhakika wa kuishi katika maisha bora.