Mwapongo (kushoto) akiwa na kada wa Chama Cha Mapinduzi (kushoto), kulia ni meneja wake wa kampeni, Lucy Mbutolwe.
WAKILI Mwandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Godwin Mwapongo, ametangaza nia ya kuwania urais wa Tanzania mwaka 2015.Wakili huyo ametangaza nia yake hapo jana katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam ambapo tayari alikuwa amekwishakuchukua fomu ya urais aliyoionyesha kwa wananchi.
Alisema aliamua hivyo ili kuijengea nchi misingi imara ya umoja, amani na maadili mema na kupambana na rushwa.
Aliongeza kuwa endapo atateuliwa atahakikisha anapambana na umaskini kuboresha elimu, afya na kumwezesha mtu wa kipato cha chini awe na uhakika wa kuishi katika maisha bora.