Uchaguzi mkuu wa Rais mwaka 2015 utakuwa wa aina yake kufuatia matukio makubwa matatu makubwa kukoleza safari ya kumtafuta rais ajaye kwa kipindi kingine cha miaka mitano.
Matukio hayo ni pamoja na (a) Vyama vya Upinzani kuungana (b) Waziri mkuu wa zamani CCM kuhamia Upinzani-Edward Lowassa (c) Vijana wengi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura.
Matukio hayo matatu yamebadilisha siasa za Tanzania kwa mwaka huu huku kujitokeza kwa vijana kujiandikisha kuna ashiria mwamko mkubwa walio nao hivisasa katika kuhakikisha kuwa wanatumia vizuri haki yao ya kikatiba ya kupiga kura tarehe 25 mwezi oktoba mwaka 2015.
Watalaamu mbalimbali wa masuala ya kisiasa nchini na nje ya nchi wamebainisha kuwa uchaguzi wa mwaka huu umekuwa tofauti na chaguzi za miaka ya nyuma hivyo basi mabadiliko hayo yanaonesha kukua kwa demokrasia ambayo inasema kwamba Wananchi wote ni sawa mbele ya sheria na wanashiriki katika kufanya maamuzi ya kitaifa juu ya masuala ya umma kwa kufuata misingi ya katiba ya nchi.
Utafiti mdogo uliofanywa na Mpekuzi umebaini kuwa wagombea wawili wamekuwa katika mchuano mkali miongoni mwa wananchi mbalimbali ndani na nje ya nchi.
Wagombea hao ni yule wa Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli pamoja na Edward Lowassa kupitia umoja wa katiba ya wanchi yaani UKAWA.
Wagombea hao ni yule wa Chama Cha Mapinduzi Dk. John Pombe Magufuli pamoja na Edward Lowassa kupitia umoja wa katiba ya wanchi yaani UKAWA.
Katika mitaa mbalimbali hivisasa Vijana wana msemo wao unaosema “Habari ya mjini”, hivyo habari ya mjini hivisasa ni Lowassa na Magufuli kugombea urais.
Katika moja ya mtaa jijini Dar es salaam mwandishi wetu ameshuhudia mabishano makali ya nani zaidi kati ya Lowassa na Magufuli huku kila upande ukitamba mgombea wake ni zaidi ya mwingine.
Kwa kiasi kikubwa mabishano hayo yamekuwa hasa upande wa utendaji serikalini pamoja na kukubalika kwao kwa ujumla katika jamii pamoja na sera za kila chama kwa maslahi mapana ya Taifa la Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Inadaiwa kuwa kuna baadhi ya maeneo ukimsema vibaya mmoja wa hao wagombea wawili ambao ni Lowassa na Magufuli unaweza ukaambulia kipigo.