Monday, September 28, 2015

Ninayo list ya kikosi cha Taifa Stars kitakachoikabili Malawi October 09 2015 …!!

Kocha msaidizi wa timu ya taifa ya Tanzania Hemed Morocco ametangaza kikosi chaTaifa Stars kitakachoingia kambini siku ya October 01 2015… Morocco ametangaza kikosi hicho baada ya kocha mkuu wa timu hiyo  Charles Boniface Mkwasa kupatwa na msiba wa mkwe wake hivyo yupo katika shughuli za mazishi.
Taifa Stars inaingia kambini kujiwinda na mechi ya kuwania kucheza Kombe la Dunia, mchezo ambao utapigwa katika dimba la uwanja wa Taifa Dar Es Salaam October 09 2015 kuikabili Malawi, hii itakuwa ni mechi yake ya kwanza ya kuwania tiketi ya kufuzu michuano hiyo.
Wachezaji walioitwa Taifa Stars ni:
Magolikipa
  • Ally Mustapha
  • Aishi Manula
  • Said Mohammed
Mabeki:
  • Nadir Haroub
  • Kelvin Yondani
  • Mohammed Hussein
  • Hassan Isihaka
  • Juma Abdul
  • Shomary Kapombe
  • Mwinyi Haji
Viungo:
  • Himid Mao
  • Said Ndemla
  • Salum Telela
  • Frank Domayo
  • Mudathir Yahaya
  • Simon Msuva
  • Deus Kaseke
Washambuliaji:
  • Rashid Mandawa
  • John Bocco
  • Mrisho Ngassa
  • Mbwana Samatta
  • Thomas Ulimwengu
  • Farid Mussa