Thursday, October 1, 2015

USHABIKI WA SIMBA NA YANGA NJEMBA APAKWA VIPODOZI LIVE

Njemba huyo akipakwa lipstick.AHADI ni deni! Njemba mmoja mkazi wa Mbezi Manyema, jijini Dar aliyejulikana kwa jina la Omar Msambaa, hivi karibuni alijikuta akipakwa lipstick, kunyolewa nywele na baadaye kuogeshwa kwa soda aina ya mirinda, ikiwa ni kutimiza ahadi yake ya awali kuwa afanyiwe hivyo endapo timu aliyokuwa akiishabikia itafungwa.