Sunday, February 7, 2016

Kama ulikosa kuangalia magoli ya mechi ya Chelsea Vs Man United, yapo hapa

Ligi Kuu Uingereza imeendelea tena leo February 7 kwa michezo miwili kupigwa, AFC Bournemouth walikuwa wenyeji wa Arsenal katika uwanja wao wa nyumbani, wakati Chelsea  walikuwa wenyeji wa Man United katika dimba lao la Stamford Bridge, mchezo ambao ndio uliteka hisia za mashabiki wengi wa Ligi Kuu Uingereza.
30F95B4A00000578-3436105-image-a-31_1454864669302
Chelsea ambao bado wapo katika kipindi cha mpito chini ya kocha wao wa muda Guus Hiddink, wamefanikiwa kutoa sare ya goli 1-1, baada ya Man United kufunga goli la uongozi dakika ya 61 kupitia kwa  Jesse Lingard, wakati Man United wakiwa na matumaini ya kuondoka na point tatu, Chelsea walifanikiwa kusawazisha goli dakika ya 90 kupitia kwa Diego Costa na kufanikiwa kumaliza mchezo kuambulia kugawana point moja moja.
30F9147000000578-0-image-a-31_1454861404849
Kwa matokeo hayo Man United wapo nafasi ya 5 wakiwa na point 41 katika michezo yao 25 waliocheza ya Ligi Kuu Uingereza hadi sasa, wakati Chelsea wapo nafasi ya 13 na point 30 wakiwa wamecheza michezo 25.
Video ya magoli ya Diego Costa na Jesse Lingard.