Thursday, March 31, 2016

Breaking Newz:Waziri Wa Rwanda Afia Gerezani Burundi

http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2015/04/27/150427110213_bujumbura_protests_640x360_getty_nocredit.jpg
Waziri wa zamani wa Rwanda Jacques Bihozagara amefariki katika gereza moja nchini Burundi miezi minne baada ya kukamatwa kwa tuhuma za kufanya ujasusi.

Rwanda imesema marehemu Jacques alikuwa ameshikiliwa kinyume cha sheria na Balozi wa nchi hiyo nchini Ubelgiji ameandika na kusema kushikiliwa kwa Jacques na kuita ni kifo cha mauaji.
Wafungwa katika gereza alipokuwa ameshikiliwa wanasema alionekana akiwa katika hali nzuri na kwamba alifariki dakika chache baada ya kuchuliwa katika gereza kupelekwa hosptali baada ya kuugua.
Umoja wa Mataifa umekuwa ukiishutumu Rwanda kwa kujaribu kuipindua serikali ya Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza, madai ambayo Rwanda imekuwa ikiyakanusha.