Tuesday, March 1, 2016

Shamsa: Siwezi kumhukumu Nay

11848861_1018939518178469_94676888_n
Staa wa Bongo Muvi, Shamsa Ford.
Showbiz
STAA wa Bongo Muvi, Shamsa Ford kwa mara ya kwanza ameibuka na kuiongelea Ngoma ya Shika Adabu Yako iliyoimbwa na Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kuwa kamwe hawezi kumhukumu Nay kwa maneno aliyoimba.
nay-na-shamsha
Shamsa Ford akiwa na  Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.
Akigonga mbili-tatu na Showbiz, Shamsa aliyewahi kubamba na Filamu ya Chausiku alisema kuwa aliusikia wimbo huo uliowachana mastaa wengi wa Bongo Muvi na kwamba bado hajajua kinachomfaidisha Nay kupitia wimbo huo.
“Namuacha kama alivyo na kamwe siwezi kumhukumu kwa kile alichokiimba labda kwa upande wake aliona ni sawa,” alisema Shamsa.
Katika Wimbo wa Shika Adabu Yako, Nay amewachana mastaa wa Muziki na Bongo Muvi ambao ni Shetta, Ommy Dimpoz, Ray, Niva, Wema Sepetu na wengine wengi jambo lililosababisha Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kuufungia wimbo huo kutokana na ukiukwaji mkubwa wa maadili, kashfa, uchochezi na kudhalilisha watu.