Friday, June 3, 2016

Magufuli ataka wanaopita kwenye barabara za mwendokasi zichomolewe tairi za magari yao na ziuzwe


Rais John Pombe Magufuli amechukizwa na uharibifu na matumizi mabaya ya miundombinu ya mabasi ya mwendo kasi na kuagiza mamlaka zinazohusika ziwachukulie hatua kwa wasiofuata sheria.

Akiongea wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa Maktaba ya kisasa Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Rais John Pombe Magufuli amevitaka vyombo vya sheria kuwachukulia hatua kali baadhi ya watu wanaohujumu miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akizungumza kuhusu barabara za mwendokasi, Magufuli ametaka wayakamate magari yanayopita kwenye barabara za mwendokasi na yapelekwe kituoni kisha wachomolewe tairi za magari yao na yauzwe na watakuwa wamepata biashara.