Monday, August 25, 2014

LUCY KOMBA AFUNGUKA JUU HARUSI YAKE NA MZUNGU ....SHEREHE KUFANYIKA MTONI

Dada Lucy hongera kwa kuwa na kipaji, kiukweli unaweza, kubwa napenda kuijua historia yako kwa ufupi. Thabiti Kiula, Igunga, 0786947474
Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Lucy Komba akipozi.
LUCY: Mimi ni mama wa mtoto mmoja wa kiume. Nimezaliwa Dar katika Hospitali ya Lugalo. Nina elimu ya kidato cha nne baada ya hapo nikasomea mambo ya usekretari. Mimi ni mwajiriwa wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Sanaa nimeanza mwaka 2010 kwenye Kundi la Fukuto Art Professional.
USHAURI
Hongera dada Lucy, nakushauri ukaze buti, naikumbuka sana muvi uliyocheza na Dk. Cheni na Mzee Magali. Jofu Mwaik, Dar, 0782780264
LUCY: Sijawahi kucheza muvi na Cheni ila ni tamthiliya tu. Mzee Magali ni kweli nilishawahi kucheza naye filamu.
NDOA
Dada Lucy ndoa yako itafanyika mwaka gani? Lee Cantana, Mwanza, 0753369500
LUCY: Mwaka huu.
WABONGO
Hivi dada kwa nini umeamua kuwatosa Wabongo wenzako na kuamua kuwa na Mzungu? Amiri Salumu, Dar, 0653252416
LUCY: Ni mapenzi tu kwani hayaangalii sura, kabila wala dini.
MATARAJIO
Lucy kiukweli mimi nakuzimia sana uigizaji wako mzuri kunako tasnia ya filamu Bongo, je, nini matarajio yako ya baadaye kuhusiana na usanii? Salim Liundi, Dar, 0659601205
LUCY: Siwezi kusema matarajio yangu ni nini maana natarajia kuhama nchi.
Lucy Komba akiwa na mpenzi wake wa mamtoni.
YEYE NA KEPTENI KOMBA WAKOJE?
Lucy eti una undugu na Kepteni Komba na je, wewe ni Mngoni? Muddy Madiley, 0652672805
LUCY: Ni ukoo tu vilevile ni Mngoni mwenzangu.
HARUSI
Napenda kujua kama harusi yako itafanyika hapa Bongo au mamtoni kwa jamaa? Brosco, Mwanza, 0685244622
LUCY: Harusi ni hapahapa, mamtoni tutaenda kumalizia sherehe.
SWALI
Hivi Lucy ulishawahi kuandika filamu yako mwenyewe na kama umewahi inaitwaje? Muddy, Dar, 0755462633
LUCY: Asilimia kubwa ya filamu zangu huwa naandika mwenyewe kama Fedheha, Kipenzi Changu, Cleopatra na nyingine nyingi.
TASNIA INAKUFA?
Sekta ya filamu Tanzania inaonekana inaelekea kufa, unafikiri nini tatizo? Elia, Iringa, 0762431001
LUCY: Tatizo ni wasambazaji kwani ni wabaguzi hawaangalii nani anafanya filamu nzuri bali wanaangalia kujuana tu.
KAFUATA PESA KWA MZUNGU?
Dada Lucy upo vizuri kwenye fani, hongera kwa kumpata Mzungu ila mbona kama watu wanaponda eti hakuna ‘real love’ hapo bali umefuata mkwanja, je, wewe unalichukuliaje hili au ndiyo wale vijiba vya roho? Rocky, Moshi, 0715289337
LUCY: Ni majungu tu na maneno ya watu hata kwenye khanga yapo.
URAFIKI
Wewe ni msanii mzuri, naomba uwe rafiki wa kubadilishana mawazo, kama upo tayari naomba unitafute. Irene, Tanga, 0657146670
LUCY: Nashukuru, nitakutafuta.
AKIOLEWA ATAHAMA?
Je, huyo Mzungu akikuoa utakwenda kuishi kwao au mtabaki hapa Tanzania? Loth, Moro, 0788133987
LUCY: Nitaenda kwao.
ALIMUIBUA WOLPER?
Wewe ni mwigizaji mkongwe, je, ni kweli wewe ndiye ulimuibua (Jacqueline) Wolper kwenye fani ya uigizaji? Ebeshente, Dar, 0757174278
LUCY: Ndiyo, asante.