Wednesday, September 3, 2014

JUMBA LA BIG BROTHER LINAUNGUA MOTO, SHINDANO SASA KUHAIRISHWA

Moto mkubwa umeikumba M-Net’s Big Brother Africa Hotshots house katika Studio ya Sasani na kusababishwa kusitishwa uzinduzi wa msimu wa 9 wa Big Bother ambao ulibidi uanze tarehe 7 September siku ya Jumapili. Hakuna mtu aliyepata madhara japokua chanzo cha moto huo bado hakijajulikana na uchunguzi unaendelea.

Kwasasa kampuni ya Endemol inayotengeneza kipindi hiki inatafuta jumba jingine ambalo watakaa housemates wa msimu mpya japokua wanasema linawaingizia gharama kubwa kimiundombinu na kufunga mitambo ya Camera