Friday, October 31, 2014

LADY JAY DEE AZUNGUMZIA HAPA WIMBO MPYA,JINA JIPYA LA BAND,HAKUNA KULIA TENA NA MOG.

Nimebahatika kukutana na Komando Lady Jay Dee leo mchana na amejibu maswali kadha kuhusu Nyumbani Lounge na Binti Mchozi [Machozi Band ]


Jide amesema "kwa sasa hakuna Nyumbani Lounge ila patakuwa panaitwa MOG Na show zake na The Band zitakuwepo kama kawaida, Machozi Band kwa sasa itajulikana kama Lady Jaydee and the Band tu"

Jide pia ameniambia kuwa "Tumeondoa kulia lia so mimi sio machozi tena, itabaki Komando na anakonda"

Lady jay Dee ameniambia kuwa November mwishoni atatoa wimbo alioupa jina "Forever" na kashirikishwa mdogo wake Dabo ambaye ni msanii we reggae hapa Tanzania. Wimbo umefanyika Combination Sounds kwa Man Water.