Friday, December 12, 2014

Maneno ya Idris kuhusu alichokiandika Davido baada ya ushindi wa Tanzania BBA

.
.
Jumapili ya Des 7 ni  siku iliyochukua headline kwenye mitandao baada ya Davido kuwakwaza watanzania kwa kile alichokiandika kwenye twitter.Baada ya Mwakilishi kutokea Tanzania Idris Sultan kutangazwa kuwa mshindi wa Big Brother Africa Hotshots.
Mengi yamezungumzwa na watu,lakini leo Des 11 mshindi wa Big Brother Africa Hotshots,Idris Sultan alipata nafasi ya kuzungumza na vyombo vya habari mbalimbali miongoni mwa maswali aliyouliza ilikuwemo ile ishu ya Davido.
Mwandishi:Idris ukiwa kama mshindi wa BBA unazungumziaje ujumbe wa Davido uliowakwaza watumiaji wa mitandao?
Idris Sultan:Kwanza ningependa kusema nahisi ilikuwa ni utani kwasababu mwishoni mwa ile sentensi kumbuka kuna alama ya utani yaani ‘Lol’ sasa nimeshangashwa kuona watu wanaanza kuhisi vibaya kuwa ni dongo kwetu hapana.Ningewataka watanzania pamoja na Davido tusiingie kwenye migogoro isiyokuwa na msingi sisi sote ni bado vijana tunatakiwa kujitangaza na kupeana support  hata vizazi vinavyokuja vijifunze vitu vizuri kutoka kwetu ikiwemo Upendo na Amani  kati ya Tanzania na Nigeria’Alisema Idris Sultan.
Hizi ni baadhi ya picha kutoka kwenye mkutano huo
.
Idris akizungumza na vyombo vya habari.
.
.
.
Vyombo vya Habari.
.
Aliyekuwa mwakilishi wa Tanzania katika shindano la BBA akizungumza na Waandishi wa Habari.
.
Meneja Masoko wa kampuni ya Multichoice Furaha Samalu akizungumza na Waandishi Habari kuhusiana na huduma za DSTV.
.
.
.
Idris Sultan akiwa na Meneja uhusiano wa kampuni ya Multichoice Tanzania,Barbara (kushoto) na Meneja Masoko wa kampuni  hiyo Barbara .
.
.
.
.
.
Idris akifanya mahojiano na Ayo TV,DSTV pamoja na Clouds TV.
.
Maripota wangu wa nguvu (Kulia) Edwintza255 & Beka wakipiga picha aina ya Selfie na wakilishi wa BBA 2014 Irene na Idris  Sultan.