Saturday, December 20, 2014

ROSE MUHANDO AELEZA ALIVYOBAKWA NA RAFIKI YAKE.....!!

SIJUI kama umeyasikia ya hivi sasa yake Rose
Muhando. Na kama hujui basi mwanamuziki
huyo maarufu wa kete za injili kutoka
Tanzania, amefunguka mazito akisema kuwa
aliwahi kubakwa.
Nyota huyo wa Bongo akifanya mahojiano na
gazeti la Amani la Tanzania hivi majuzi,
alisema kuwa yule aliyemtendea unyama huo
alikuwa ni mtu wa karibu sana naye.
“Dunia ina mambo mengi sana ndugu
zanguni, wengine wema, wengine waovu. Mimi
nakumbuka siku moja kuna mwanaume
ambaye nilikuwa na ukaribu naye. Huyu
bwana, ana jina kubwa sana Dodoma.
Alinichukua kwenye gari kwa ajili ya kunisaidia
mambo fulani maana alikuwa ananisaidia
katika kazi zangu,” alitanguliza.
“Nilishangaa kumuona anapeleka gari nje ya
mji, nikamuuliza tunakwenda wapi, akasema
tulia utajua. Sikuwa nimemuwazia ubaya,
hivyo nilitulia lakini matokeo yake akanipeleka
hadi porini ambako alikutana na watu
wengine, naamini walikuwa wasaidizi wake”.
“Wale watu wakaniweka chini ya ulinzi na
kunifunga kamba kisha wakanioneshea mtutu
wa bastola, nami nikasalimu amri na
wakanitendea unyama huo wa kunilazimisha
mapenzi” alisema Rose huku akisisitiza ni
tukio ambalo hawezi kulisahau.
Licha ya kuwa alipiga ripoti polisi, Muhando
amedai kuwa anaogopa kuanika jina la mbakaji
huyo waziwazi kwani anahofia usalama wake
kwa sababu ni mtu mwenye ushawishi
mkubwa.