Friday, January 2, 2015

ACHOMWA KISU KICHWANI NA KUTEMBEA NACHO KWA ZAIDI YA MASAA MAWILI AKIENDA HOSPITALI!!

 
Mwanaume mmoja Brazil amewashangaza wengi baada, ameweza kutembea masaa mawili kuelekea hospitali akiwa na kisu kichwani alichochomwa na majambazi waliomvamia akiwa anatoka Club. 
Kisu hicho kilizama kichwani kwa urefu wa 30cm kilimpata mwanaume huyo Juacelo Nunes pembeni ya jicho la kushoto na kutokea kwenye shavu wakati akipambana na majambazi hao.
“Kisu kilipita katika baadhi ya mishipa yake ya damu ambayo ingeweza kumuua kutokana na kuvuja kwa damu nyingi,” alisema daktari Gilberto Albuquerquealiyemhudumia mgonjwa huyo kutoka hospitali ya Teresina alipofikia kupata matibabu.
Kisu hicho kilitolewa na kukabidhiwa Polisi ambao wanaendelea na uchunguzi kuwatafuta wahusika wa tukio hilo.


Daktari amesema mgonjwa huyo kwa sasa yuko chini ya uangalizi wa madaktari na hali yake inaendelea vizuri.